MWANZO WA WAHY

Amesema Bukhari na Muslim na wengineo kuwa: Imepokewa kutoka kwa Azzuhry naye amepokea kwa U'rwa bin Zubeir naye amepokea kwa Mwana Aisha (mkewe Mtume) kwamba: Malaika Jibril (a.s) alikuja kwa Mtume (s.a.w.) naye akiwa katika pango la Hiraa akamwambia: Soma, Mtume akajibu: Mimi sijui kusoma. Mtume anasema: Malaika akanikaba kwa nguvu mpaka nikazidiwa kisha akaniambia: Soma, Mtume akajibu: Mimi sijui kusoma. Kisha ndipo Malaika alipomsisitiza kwa nguvu akisema:
"Soma kwa jina la Mola wako, ambaye ameumba. Amemuumba mwanadamu kutokana na damu iliyoganda. Soma na Mola wako ni Mtukufu kuliko wote". Qur'an, 96:1-3
Baada ya hapo, Mtume (s.a.w.) alirudi kwa mkewe mwana Khadija (a.s.) akiwa amejawa khofu kubwa. Alipoingia ndani alijitupa chini na huku akilalamika: "Nifunikeni, nifunikeni!!" Alipotulia akasema: "Ninaogopa sijui kitanipata nini?!" Khadija akamtuliza: "Sivyo! Wallahi Mwenyeezi Mungu hatakuangamiza abadani, wewe unaunga udugu, unavumilia matatizo, unasaidia wanyonge, unasaidia kuleta haki." Hapo Khadija akamchukua Mtume akampeleka kwa Ibnu ammi yake Waraqa bin Nawfal (alikuwa mnasara, mwandishi wa Injili kwa lugha ya kiibrania).
Walipofika kwa Waraqa, Khadija akamwambia: "Ewe Ibnu ammi! Msikilize Muhammad aliyo nayo." Waraqa akamuuliza, "una nini?" Muhammad (s.a.w.w) akamwelezea yote kama aliyoyaona, Waraqa akamwambia: "Huyu ni Malaika ambaye amepata kumteremkia vilevile Nabii Musa (a.s.) Ee!!!" Natamani kama nitakuwa hai wakati watakapokufukuza watu wako!!! Muhammad (s.a.w) akashituka: "Watanifukuza??" Waraqa akajibu: "Ndiyo, hakuna mtu yeyote anayeleta jambo kama hili uliloleta wewe isipokuwa atapigwa vita na watu wake".
Taz: Sahihi Bukhari J.I uk, 5-6
Sahihi Muslim J. I uk, 97
Almuswannaf J. 5 uk, 322
Tarikhut Tabari J. 2 uk, 47
Enyi waislamu wenzangu, mnaaminije hadithi hizi zenye kumshusha hadhi Mtume wetu kwamba yeye alikuwa hajuwi kuwa yeye ni Mtume wa Allah mpaka aende kuambia na mkristo? Je hii inaweza kuwa kweli? Story hii inamdhalilisha hata Jibril kwani tukikubali hadith hizi itamaanisha kuwa Jibril ambaye anajulikana kuwa mwalimu wa mitume wote alimbana na kumtesa mtume bila hata kumwambia yeye ni nani na wala hakujitambulisha.

Sisi Mashia tunaamini kuwa Jibril alipomtokea Mtume alijitambulisha kwake na pia Yeye mwenyewe Mtume Mohammad (s.a.w.w) alijijua kuwa ni mtume na wala hakuhitaji kwenda kuamiwa na wakristo kuwa wewe ni Mtume ndio woga aliokuwa nao ukaisha. Wewe unasemaje?

Comments