NURU TUKUFU YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W.W.)
1. Sheikh Shahabuddin Qastalani katika
kitabu chake Mawahib al- Ladunniyyah ameandika hivi:- Alipokusudia Mwenyezi
Mungu kuwaumba viumbe vyake, aliichomoza
Nuru ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.); Nuru ambayo ni tukufu ndipo akaumba dunia.
2. Amehadithia Bwana Jabir bin Abdullah
Ansari: “Nilipomwuliza Mtume Muhammad (s.a.w.w.) ‘Ya RASUL-ALLAHI wazee wangu
nakufidia, ni julishe kiumbe yupi
aliumbwa mwanzo?’. Akanijibu ‘Ewe Jabir, Mwenyezi Mungu aliumba nuru ya Mtume
wake kutokana na nuru yake kabla ya
kuumba chochote’”.
3. Na vile vile Sayyidna Ali (a.s.)
ameeleza kwamba mpenzi wa Mwenyezi Mungu Mtume Muhammad (s.a.w.w.) amesema:
“Mwenyezi Mungu ameumba nuru yangu miaka kumi na nne elfu kabla ya kumuumba
Nabi Adam (a.s.)”.
4. Mwanahistoria maarufu wa Ki-Islamu Bwana
Abul-Hasan Ali bin Husain al-Mas’udi katika kitabu chake maarufu cha historia
kiitwacho Muruj adh-dhahab wa Ma’adin
al-Jawahir, amepokea hadithi hii kutoka
kwa Imam Ali (a.s.) kwamba Mwenyezi Mungu alipotaka kuumba dunia na watu na kila kilichomo ndani
ya dunia, basi kwanza kabla hakuiumba
hii ardhi, kwa upekee kwa Nuru yake Jalali
akaidhihirisha nuru yenye kung’aa kutokana na nuru yake na ikawa ile
nuru inatoa cheche za nuru na mshabaha wa sura; tena akakusanya zile sura akaifanya sura moja na
ikatokeza sura ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.), basi hapo Mwenyezi Mungu
akaikhutubia ile sura na kusema “Wewe ndiye niliyekuchagua, na wewe ndiye nuru
yangu, kwako wewe nimewacha hazina ya uwongofu na kwa ajili yako (kwa mapenzi
juu yako) mbingu nitainyanyua; na ardhi (dunia)
nitaitandaza na maji nitawacha yamiminike na yaende; na kujaalia thawabu
na adhabu, Pepo na Jahannam (Moto) kwa watii na wasiotii; na nitawafanya Aali
yako (AHLUL-BAYT) kuwa viongozi wa Haqi, na nitawajaza kwa elimu hata
wasishindwe kueleza au kuwafahamisha Umma mushkili wowote wala jambo lolote
lililofichika wasishindwe kulieleza, na nitawafanya wao (AHLUL-BAYT) wenye Hoja
na Mfano juu ya viumbe wangu na kuwa nabihisha (kuwafahimisha upekee/
Wahdaaniyah) wangu na Qudra yangu juu ya viumbe vyote”. Baadaye Mwenyezi Mungu
akachukuwa Ahadi kwa kuyakubali yote, na kabla hakuchukua hiyo Ahadi
akawajulisha viumbe vyote kwa kumchagua Mtume Muhammad (s.a.w.w.) na Aali zake
kuwa ni viongozi wa Haqi na
wamechaguliwa naye ili iwe ndio njia ya uadilifu na viumbe wasiwe na udhuru
wowote wa kwamba hawakujua.
5. Bwana Abul Qasim al-Tabarani (360
A.H.) katika kitabu chake Muj’am
al-Kabeer anahadithia kutokana na Bwana Ibn Abbas kwamba Mtume (s.a.w.w.)
amesema: “Mimi nilikuwa Mtume wakati Adam (a.s.) alipokuwa kati ya roho na
kiwiliwili (maana yake bado umbo la Nabi Adam lilikuwa halikukamilika)”.
Huu ndio ukweli kuwa Mtume Muhammad (saww) ndio Mtu wa kwanza
kuumbwa na Mungu aliwachagua Ahlulbayt kuwa makhalifa wa Mtume kabla hata ya
dunia kuumbwa. Hapa hakuna Abubakar wala Umar. Makhalifa ni Ahlulbayt tu. Na jumla
ya makhalifa ni 12. Wa kwanza wao akiwa ni imam Ally na wa kumi na mbili wao ni
imam Muhammad Mahdi (a.s).
Comments
Post a Comment