UTARATIBU WA KUWASULUHISHA
WATU
Wakati fulani, enzi za Imam
Sadiq (a.s), Abu Hanifa, mtawala wa Hajjaaj, alikuwa na ugomvi na mkwe juu ya
urithi. Mufadhal Ibn U’mar Kufi, mmoja wa masahaba wa karibu wa Imam Sadiq
(a.s) alipita kwenye ugomvi huo. Aliposikia mabishano hayo alisimama na kusema
kuwaambia hao wanaume wawili: “Twendeni nyumbani kwangu.” Walifanya kama alivyoomba.
Walipofika nyumbani aliingia
ndani na muda mfupi baadaye alitoka na mfuko wenye dirhamu mia nne alizowapatia
(hao) watu wawili na akawasuluhisha. Kisha akaeleza: “Hizi sio fedha zangu bali
ni za Imam Jaafar Sadiq (a.s). Alinielekeza: “Wakati wowote utakapoona shia
wetu wawili wakizozana juu ya fedha, wapatie fedha hizi na wasuluhishe.”
Comments
Post a Comment