SALA YA ASUBUHI

SALA YA ASUBUHI 

1. Baada ya kusema Iqamah, utanuwia sala kama hivi:-
Nasali Sala ya Asubuhi Rakaa mbili kurbatan ilallahi Taala
2. Utasema' Allahu Akbar'
3. Utasoma sura ya Al-hamdu:
BISMILLAHIR RAHMAANIR-RAHIM. ALHAMDU LILLAHI RABBIL – ALAMIIN. ARRAHMANIR RAHIIM. MAALIKI YAWMIDDIIN. IYYAKA NAABUDU WAIYYAKA NASTAIIN. IHDINAS SIRAATWAL MUSTAQIIM, SIRAATWA LLADHIINA AN’A AMTA ALAYHIM, GHAYRIL MAGH-DHUBI ALAYHIM WALADH - DHWAALLIIN.
Tafsiri yake ni kama hivi:
Kwa jina la Allah Mwenye rehema za dunia na rehema za Akhera.
Kila sifa nzuri inamstahili Alla {Mungu} mlezi wa viumbe vyote.
Mwenye rehema za dunia na akhera.
Mfalme wa siku ya Kiyama.
Wewe tu ndie tunae kuabudu, na wewe tu ndio tunae kuomba msaada.
Tuongoze katika njia iliyo nyooka sawa. Njia ya ambao ulio waneemesha, isiokuwa ya wale ulio waghadhibikia juu yao wala wale walio potea.

4. Baadae utasoma, sura nyingine yoyote kamili.
ni bora usome sura ya Tawheed:
BISMILLAHIR RAHMANIR RAHIIM
QUL HUWA LLAHU AHAD. ALLAHUS SWAMAD. LAM YALID WALAM YUULAD. WALAM YAKULLAHUU KUFUWAN AHAD.
Tafsiri yake ni kama ifuatavyo:-
Kwa jina la Allah Mwenye Rehma za dunia na Rehma za Akhera
Sema, yeye Mungu ni mmoja. Mungu, Asiye hitaji, ambaye wote wanahitaji kwake.
Hakuzaa wala hakuzaliwa. Wala hakuwa anaye fanana naye hata mmoja.
5. Kisha utasema' Allahu Akbar' na utainama mpaka vifike viganja vyako magotini, utaweka juu yake na utasema:-
SUBHANA RABBIYAL – ADHWIMI WA BIHAMDIHI
ALLAHUMMA SWALLI ALA MUHAMMADIN WA AALI MUHAMMAD
{Ninamtukuza Mola wangu Aliye mkubwa na ninataja sifa zake njema}
{Ewe Mwenyezi Mungu, Mrehemu Muhammad na Ahli zake.}

6. Kisha utanyanyua kichwa chako na utasimama, na kusema:-
Samiallaahu liman Hamida. Allahu Akbar.
{Mwenyezi Mungu Anamsikia kila anayemshukuru}.

7. Kisha utasujudu; utawekapaji lako la uso juu ya kidongo twahara au mfano wake, na hivyo hivyo utaweka vitanga vyako na magoti na vidole gumba vya miguu ardhini, na kusema:-'SUBHANA RABBIYAL A'LA WABIHAMDIHI ALLAHUMMA SWALLI ALAA MUHAMMADIN WA AALI MUHAMMAD'
{Nataja Utukufu wa Mwenyezi Mungu, Bwana wangu alie juu ' kabisa, na ninamshukuru}.

8. Kisha utanyanyua kichwa chako na kukaa, na kusema: -
ALLAHU AKBAR, ASTAGH FIRU LLAHA RABBI WA ATUBU ILAYHI, ALLAHU AKBAR'
{Naomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu, Bwana wangu, na ninatubu kwake}.'

9. Kisha utasujudu sijda ya pili kama ya mwanzo, utakaa baada yake,
kisha utasimama kwa Rakaa ya pili, utasema utaposimama.
BIHAULILLAHI WA QUWWATIHI AQUMU WA AQ-UD
{Kwa msaada na nguvu ya Mwenyezi Mungu nainuka na nakaa.}

10. Baada ya kusimama kutoka Rakaa ya kwanza, utasoma sura ya Al-Hamdu na sura nyingine katika Rakaa ya pili kama ulivyosoma katika Rakaa ya kwanza.

11. Baada ya kusoma Al-Hamdu na sura, utaomba Dua na kunyanyua mikono mkabala wa uso, na utasema:-
'RABBANAA AATINA FIIDDUN’YAA HASANATAN WA FIL AAKHERATI HASANATAN WAQINA ADHABAN-NAR.'
{Ewe Mola wetu; Tupe hapa duniani kila yaliyo mema, na utupe Akhera kila yaliyo mema, na utukinge na adhabu ya moto.}
12. Kisha utarukuu, kama ulivyofanya katika Rakaa ya kwanza, na utasujudu sijda mbili kama mwanzo.

13. Baada ya kukaa kutoka sijda ya pili, utasoma Tashaahud kama ifuatavyo:-
ASH - HADU AL LAA ILAAHA ILLALLAHU WAHDAHU LA SHARIKA LAHUU WA ASH - HADU ANNA MUHAMMADAN ABDUHU WA RASULUH. ALLAHUMMA SWALLI ALAA MUHAMMADIN WA AALI MUHAMMAD.
Tafsiri yake ni hii:
Nakiri kuwa hapana Mola ila Mwenyezi Mungu, yeye tu wala hana mshirika yeyote.
Na nakiri kuwa Muhammad {s.a.w.w.} ni mtumwa na mjumbe wake.
Ewe Mwenyezi Mungu mpelekee rehma Mtume wako Muhammad na Ahali zake.

14. Kishautasoma Salaam:-
ASSALAAMU ALAYKA AYYUHANNABIYYU WARAHMA TULLAHI WA BARAKATU. ASSALAAMU ALAYNA WA ALA IBADILLAHIS SALIHIIN
ASSALAAMU ALAYKUM WARAHAMA TULLAHI WA BARAKATUH.
Tafsiri yake ni kama ifuatavyo:-
Amani juu yako Ewe Mtume Mtukufu, na Rehma ya Mwenyezi Mungu na baraka zake; Amani juu yetu na juu ya viumbe wa Mungu watenda mema:
Amani juu yenu na Rehma ya Mwenyezi Mungu na Baraka zake.

15. Kisha utasema ALLAHU AKBAR, ALLAHU AKBAR, ALLAHU AKBAR.

16. Baada ya sala ni bora mno kusoma Tasbihi kama hivi: -ALLAHU AKBAR {x34} AL-HAMDU LILLAH {x33} SUB HANA LLAH {x33}

Comments