HISTORIA FUPI YA MTUME MOHAMMAD (S.A.W.W)

JINA  LAKE NA NASABU  YAKE.
Jina lake ni Mohammad bin Abdallah bin Abdul Mutwalib bin Hashim bin Abdul Manaf bin Quswai bin Kilaab. Na ukoo wake mtukufu unamalizikia kwa mtume Ibrahiim  (A.S)
MAMA  YAKE.
Mama yake ni Amina binti Wahabi bin Abdul manafi bin Zuhra bin Kilaab.
KUNIA YAKE NI:
Abul qaasim, pia Abuu Ibrahiim.
JINA LAKE MASHUHURI.
1- Mustafa, na anayo majina mengine mengi yaliyo pokelewa  ndani ya Qur’ ani tukufu kama:
2- Khaatamun Nabiyyiin. 3- Al Ummiyyi. 4-  Al Muzammil. 5- Al Mudathir. 6-  Al Mubiin. 7-Al Kariim.
8- An Nuur. 9- An Niima. 10-  Ar Rahmaan. 11- Ash Shaahid. 12- Al Mubashir.13-  An Nadhiir. 14- Abdur Rauuf.    15- Ar Rahiim. 16- Ad Daai  na mengine mengi.
TAREHE  YA KUZALIWA KWAKE.
Alizaliwa tarehe  17 mwezi wa Rabiiul awwal, mwaka  wa tembo sawa na mwaka  571 H.D. kutokana na kauli iliyo mashuhuri kwa mashia, na kauli nyingine inasema ya kuwa alizaliwa tarehe 12 mwezi wa Rabiul awwal mwaka huo huo.
SEHEMU  ALIPO  ZALIWA.
Alizaliwa katika mji wa Makkatul  Mukarramah ulioko katika nchi ya Saudi Arabia ya sasa.
KUPEWA  KWAKE  UTUME.
Ali pewa rasmi utume tarehe  27 mwezi wa rajab katika mji wa Makka baada ya kutimiza miaka  40 ya umri wake mtukufu.
MAFUNDISHO  YAKE.
Mtume (s.a.w) alikuja na wito wa usawa kwa viumbe wote, na alikuwa akilingania udugu, na msamaha kwa kila mwenye kuingia kwenye Dini ya ki islaam, kisha aliweka sheria iliyo nyepesi, na kanuni za uadilifu alizo zipokea kutoka kwa Mwenyezi Mungu alie takasika,  kisha waislaam wakazipokea kutoka kwa Mtume (s.a w).
MIUJIZA  YAKE.

Muujiza wake pekee wa milele na milele ni Qur’ ani tukufu; ama miujiza yake iliyo dhihiri mwanzoni mwa uislaam ni mingi sana kwani haihesabiki.

Comments