Bwana Ibn Athir
al-Jazari katika kitabu chake Tarikh al-Kamil anaandika
kwamba Abdi-Manaf (Babu wa tatu wa Mtume wetu (s.a.w.w.))
alikuwa na watoto wawili Abdush-Shams na Hashim ambao
walizaliwa mapacha kwa hali kidole cha mmoja wao kiligandana
na kipaji cha mwenziwe. Walipofanyiwa kupasuliwa mahali
pale paliposhikamana ikatoka damu nyingi. Wakasema watu: ‘hii
ilionyesha kwamba baina ya ukoo wao patamwagika damu nyingi’.
Aliposhika Bwana Hashim
mahala pa baba yake Abdi-Manaf kuwa yeye mkubwa wa kabila, basi Ummayah mtoto
wa Abdush-Shams akaona wivu juu yake, hivyo uadui baina ya watoto wa Hashim na Ummayah
ukaanzia hapa.
Katika kitabu cha tafsir
mashuhuri kiitwacho Durr al-Mansur cha
Jalaluddin Suyuti imeandikwa hivi kwamba Ibn Jaree, Ibn Mundhir, Ibn Abi Hatim,
Tabrani, Ibn Mardwaih na Hakim wamehadithia kwa njia sahihi mbali mbali kwamba
Ali ameeleza tafsiri ya aya hii: ‘Alam-Tara Ilal-Ladhiyna Bad-Daluu
Nia-Matal-Laahi Kufra”. (Je, hukuwaona wale waliobadilisha neema ya Mwenyeezi
Mungu kwa
kufru) (Sura Ibrahim,
Aya 28) hivi, “Wale waliobadili dini ya Mwenyezi Mungu kwa kukufuru ni wana
(watoto) wa Umayyah na watoto wa Mugheera, ambao ni wenye kubobea kwa dhambi
kuliko Quresh wote.”
Sijui itakuwaje kwa
wafuasi wao? Kumbuka Uthuman bin Afan, Muawiyah bin Sufian, Yazid bin Muawiya
n.k walikuwa bani Umayya yaani watoto wanaotokana na fitina hii iliyotajwa
katika Qur’an tukufu. Bila shaka Mawahhabi na wapende kuua wote wanatokana na
kizazi hiki au ni wafuasi wao. Mungu atuepushe kutokana na kukifuata kizazi
hiki kilicholaaniwa.
Ameen.
Comments
Post a Comment