HUU NDIO USHUJAA WA UMARY BIN KHATAB (R.A)

Tumesimuliwa masimulizi mengi juu ya Ushujaa wa Umar bin Khatab lakini ukifuatilia Historia utagundua kuwa Umar alikuwa shujaa wa kuuwa waislamu wenzake na watu wasiokuwa na hatia. Lakini anapokuwa vitani alikuwa ni mwoga kweli kweli.
Omar na wenziwe walikimbia katika vita vya Uhud, na Hunain. Pia Mtume alipomtuma katika vita vya Khaibar alirudi bila ushindi na hata katika vikosi vidogo vidogo alivyoshiriki hakupewa uongozi. Kwa mara ya mwisho aliagizwa na Mtume kuwa chini ya jeshi lililokuwa linaongozwa na kijana wa miaka 18 yaani Usamah bin Zaid bin Harith.
Umar alithubutu kumtisha Fatumah bint Rasulullah kuwa kama wasipotoka kwenda kukubali utawala wa Abubakar basi ataiunguza nyumba yake. Kama haitoshi alidiriki kuwa dhidi ya kitabu cha Allah na Sunnah za Mtume wake, akahukumu katika zama za Ukhalifah wake, hukumu zinazokwenda kinyume na Qur’an na Sunnah tukufu.
Soma:
1.     Tarikh At-Tabari na Tarikh ibn Al-Athir
2.     Al-Imamah was-Siyasah cha ibn Qutaibah
3.     An-Nas wal-Ijtihad
Uko wapi ucha Mungu wa Umar enyi watu? Kama kiongozi yuko hivi itakuwaje kwa wanaomfuata? Tafakari, chukua hatua.
Mambo mengi mazuri kumhusu Umar yaliandikwa na watu aliowaajiri ili kuhalalisha ufedhuli na dhuluma zake dhidi ya Mtume na Ahlulbayt wake na hata waislamu kwa ujumla. Lakini mtu atakayesoma vitabu kwa makini, uovu wa Umar haufichi hata ufanyeje.


Comments