IMAM ALLY (a.s) NA UISLAMU

Imam Ali alijaaliwa kuwa mkono wa kuume wa Uislamu, na ngao na kingio la Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) Takdira au maajaliwa yake yalikuwa kiungo kisichotenganishwa na takdira ya Uislamu, na maisha ya Mtume wake. Alikuwepo katika kila hali ya mambo katika historia ya harakati hii, na alishika nafasi ya kuwa nyota ndani yake. Ilikuwa, kwa dharura, ni nafasi ambayo yeye pekee ndiye angeweza kuishika. Aliakisi "taswira" ya Muhammad (s.a.w.w). Kitabu cha Allah (s.w.t.) chenyewe kimemuita "nafsi" au mwandani (nafsi ya pili) ya Muhammad katika Aya ya 61 ya Sura ya tatu, na alionyesha jina lake maarufu toka upande mmoja hadi mwengine, wa historia.

Katika miaka ijayo, muundo wa ufanyaji kazi pamoja wa Muhammad na Ali - amir na mfuasi - utakuja kuweka "Ufalme wa Mbinguni" katika ramani ya dunia, HATA KAMA WANAFIKI WANALIPINGA HILO NA KUANZISHA TAWALA ZAO ZA KUCHINJA WATU BILA HURUMA NA KUWADHALILISHA WANADAMU.

Comments