ISRA NA MIRAJ: HISTORIA YAKE

Tarehe ya tukio hili imeandikwa na wanahistoria maarufu wa kiislamu wawili Ibn Ishaq na Ibn Hisham ya kwamba ilikuwa mwaka wa 10 baada ya tangazo la utume wa Muhammad (s.a.w.w). lakin Baihaqi ameandika kuwa tukio hili lilitokea mwaka wa 12 baada ya tangazo la utume. Na wengine.
Huenda tukio hili lilitokea mara mbili, lakini tukio hili liliambatana na agizo la swala tano, bila shaka tukio hili limetokea kabla ya kifo cha mzee Abutalib aliyefariki mwaka wa kumi.

Hadith: JIWE LA JAHANAMU
Mtume (s.a.w.w) anahadithia kuwa alipokuwa mbinguni alisikia sauti ya kutisha, akauliza ndipo alipoambiwa kuwa hiyo ni sauti ya jiwe lilirushiwa ndani ya moto wa Jahanamu miaka 70 iliyopita na sasa ndio kwanza linatua chini ya Jahannamu. Kutokana na tukio hili Mtume hakuwahi kuonekana akicheka tena.
Kisha anasema tuliendelea na safari yetu ambapo nilimuona malaika aitwaye Ismail. Yeye ni mhudumu wa Khitfah ambayo Qur’an inasema kuwa baadhi ya wanaohitaji kuiba siri za mbinguni hudhibitiwa kwa ndimi za moto. Ismail ni kiongozi wa malaika wenziwe 70,000. Ismail alimuuliza Jibrail kuwa ni nani huyu? Akajibiwa huyu ni Muhammad ambaye amepewa ujumbe na Allah.

Mlango ulifunguliwa tukaingia mbinguni. Nilimsalimia na nikamuombea msamaha. Naye alinisalimia na kumuomba Allah anihurumie. Kisha akasema karibu ewe Mtume mkuu, wakati huo kundi la malaika lilinisalimia. Wote walikuwa wanatabasamu. Isipokuwa mmoja ambaye alikuwa amekaa katika muundo wa kujificha, jina lake ni Khazin ambaye alikuwa na huzuni tena akilia. Jibrail akasema kuwa huyu ndio muwashaji wa Moto wa Jahanam, tokea Mwenyezi Mungu alipomteua kuwa muwashaji wa moto wa Jahanamu hajacheka tena mpaka leo. Kila siku hasira zake dhidi ya waovu zinaongezeka na kupitia malaika huyu waovu wataadhibiwa na Allah. Nilimsalimia naye akanisalimia kisha akaniambia kuwa mimi ni mtu wa peponi, kisha aliniuliza kama ninataka kuuona moto wa Jahanamu, Jibril akasema muoneshe.
Khazin alifungua mlango wa Jahannam na moto ukasambaa mpaka angani kiasi kwamba nilidhani kuwa ndimi hizi za moto karibia zitanifikia.
Jibril alimwagiza Khazin afunike Jahanam, hivyo ikafunikwa.

Soma Bihar al-Anwar, Vol. 18, p. 320-321, Bab 3 - Ithbaat al-Mi`raaj wa ma`anaahu wa kayfiyyatuhu wa sifatuhu wa ma jaraa feehi wa wasf al-buraaq, Hadith 34.

Comments