ISRA NA MIRAJ: SIDRATUL MUNTAHA

Mtume (s.a.w.w) anaendelea kutuhadithia: tulifika eneo linaloitwa Sidratul Muntaha. Eneo hili lina mti ambao jani lake moja ni kubwa kiasi cha kufunika taifa zima. Kisha tukaenda katika eneo ambalo Allah amesema katika Qur’an kuwa … kiasi kwamba alikuwa umbali wa mita mbili au chini yake kwa ukaribu. Kisha Allah aliita,  Mtume ameamini mambo ambayo Mola wake amemfunulia.
Kwa niaba ya umma wangu niliitika, na waumini wote wanamwamini Allah, malaika wake, vitabu vyake na mitume wake, hatutofautishi kati ya Mitume. … umma wangu wanasema, … tumesikia na tunatekeleza, Mola wetu. Hivyo tunakuomba msamaha nasi tunakutegemea wewe.
Allah (S.W) akasema siwezi kukulazimisheni kufanya jambo isipokuwa linalingana na uwezo wako. Kisha nikasema, Mola wetu, usituadhibu tutakapo sahau au kukosea. Allah (S.W) akajibu, sitokuadhibuni.
Kisha nikaendelea, ewe Mola wetu, usitutwishe mzigo mkubwa kuliko ulivyowatwisha waliotutangulia. Allah akajibu, sitokutwisheni mzigo.
Nikasema kwa mara nyingine, Mola wetu usitulazimishe kufanya yale ambayo hatuna uwezo wa kuyafanya, tusamehe, tunaomba ulinzi wako na huruma yako. Hakika wewe ndio mlezi wetu, hivyo tusaidie tuweze kuwashinda makafiri.
Mwenyezi Mungu mtukufu akasema hakika hayo ndio niliyokupa wewe na umma wako.

Soma; Bihar al-Anwar, Vol. 18, p. 328-329, Bab 3 - Ithbaat al-Mi`raaj wa ma`anaahu wa kayfiyyatuhu wa sifatuhu wa ma jaraa feehi wa wasf al-buraaq, Hadith 34.

Comments