Kifo cha Mtume Mohammad (S.A.W.)

Mtume baada ya kwa miaka kumi ya kuishi mjini Madina ambapo Mtume (s.a.w.) aliugua kwa mara ya mwisho. Huu ulikuwa ni muda mbaya sana kwa familia yake. Hadhrat Ali (a.s.) alikaa karibu na Mtume (s.a.w.) kwa wakati wote wa ugonjwa wake na Mtume (s.a.w.) hakupendelea Hadhrat Ali (a.s.) aachane naye hata kwa muda mfupi tu. Hatimaye, Mtume (s.a.w.) aliaga dunia na kurudi kwa Bwana Wake. Kabla hajafa Mtume (s.a.w.) alimtaka Hadhrat Ali (a.s.) asogee karibu naye, akamkumbatia na akazungumza naye kwa muda mrefu akiwa na madhumuni ya kumpa maagizo ya mwisho. Hata baada ya Mtume (s.a.w.) kumaliza mazungumzo yake na Hadhrat Ali (a.s.) hakumwachilia aende, bali aliendelea kumshika mkono na kuuweka kifuani pake na roho ya Mtume (s.a.w.) ilipotoka mkono wa Hadhrat Ali (a.s.) ulikuwa bado upo kifuani pake.

Comments