Katika mwaka wa kumi Hijjra, Mtukufu Mtume (s.a.w.) alipeleka jeshi kwenda
kupigana Roma. Katika jeshi hilo Mtume aliamuru liongozwe na Usama bin Zaid (R.A)
akasema:- "Nenda ukapigane alikouliwa baba yako". Uteuzi huu Masahaba
haukuwapendeza, kwa hiyo walisikika wakipinga amri hiyo wakisema:
"Itakuwaje mtoto mdogo huyu apewe madaraka makubwa juu yetu?
Ilipomfikia habari hii Mtume (s.a.w.)
aliwaambia: "Nimesikia lawama zenu nilivyomtawalisha Usama katika jeshi
hili, sioni ajabu, maana mlikwisha nilaumu zamani nilipomtawalisha baba yake
kabla yake. Wallahi baba yake alikuwa ni mtu aliyefaa kushika uongozi wa jeshi
hilo, kama ambavyo mtoto huyu anastahiki kabisa uongozi wa jeshi hili".
Mtume (s.a.w.) akasisitiza watu wote isipokuwa Ali, waende na jeshi Ia Usama
akisema: "Andaeni jeshi la Usama, Mwenyezi Mungu amlaani atakaebaki
asiende na jeshi hilo".
Tazama:
AI-miIalu Wannihal Juzu ya 1 Ukurasa wa 20.
Alipofika nje kidogo ya mji, Usama aliweka
kambi ili watu wakusanyike pamoja tayari kwa msafara. Hapo Abubakar akaanza
kumshawishi Usama kwamba asipeleke hilo jeshi kwa sababu haiwezekani kutoka na
kumwacha Mtume (s.a.w.) akiwa hali hii ya maradhi. Abubakar alikuwa ni mtu
mzima kwa umri kuliko Usama, takriban umri wa Abubakar wakati huo si chini ya
miaka hamsini, na umri wa Usama si zaidi ya miaka Kumi na Tisa.
Abubakar alitumia hila mbali mbali kwa kuendesha majadiliano kati yake na kijana mdogo Usama, baina ya jeshi liende kupigana Roma kama alivyoamuru Mtume, au lisiende kama anavyotaka Abubakar. Hali hii ilichelewesha na kuchukua muda mrefu bila ya kwenda alikoamrisha Mtume, mpaka mauti yakamfikia akafa Mtume (s.a.w.).
Abubakar alitumia hila mbali mbali kwa kuendesha majadiliano kati yake na kijana mdogo Usama, baina ya jeshi liende kupigana Roma kama alivyoamuru Mtume, au lisiende kama anavyotaka Abubakar. Hali hii ilichelewesha na kuchukua muda mrefu bila ya kwenda alikoamrisha Mtume, mpaka mauti yakamfikia akafa Mtume (s.a.w.).
Mwenyezi Mungu anasema: "Haiwi
kwa mwanamume aliyeamini wala kwa mwanamke aliyeamini, Mwenyezi Mungu na Mtume
wake wanapohukumu jambo lo lote wawe na khiari katika hukumu hiyo. Na mwenye
kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hakika amepotea upotevu ulio wazi"
(Qur’an 33:36).
Amri aliyohukumu Mtume hapa ni Usama kuwa Mkuu
wa jeshi litakalokwenda kupigana Roma, matokeo ni kwamba; baadhi ya Waislamu
hawakutii amri hiyo. Katika Aya, iliposema: "Na mwenye kumuasi Mwenyezi
Mungu na Mtume wake, hakika amepotea upotevu ulio wazi." Hapa Abubakr na
Umar wanapatikana na hatia ya kumuasi Mtume (s.a.w.), na mwenye kumuasi Mtume
amemuasi Mwenyezi Mungu.
Sasa jiulize, wale wanaozua visa vya uongo ili
kutetea matendo ya watu hawa wako katika kundi gani kama sio kuwekwa kundi moja
na viongozi hao. Kwa hakika watu hawa wanafuata maelezo ya watangulizi wao bila
ya kuyafikiri kwa kina. Enyi waislamu tusifuate isipokuwa yaliyoyanayokubaliana
na Qur’an na ukweli wa mambo na wala sio matamanio yetu. Ukweli ni kuwa hata
mimi nilitamani sana kuwatetea mabwana hawa lakini ukisoma historia huwezi
kupata mwanya wa kuwatetea
Comments
Post a Comment