MASHEIKH WA KISHIA WAWAPINGA MAWAHHABI WANAODAI KUWA QUR’AN INAMAPUNGUFU

 (1) al-Fadhl bin Shaadhaan: Huyu ni kati ya wanazuoni wakubwa wa Kishia aliyeishi katika karne ya tatu ya Hijria. Katika kitabu chake kiitwacho al-lidhaah, katika kukataa baadhi ya maoni ya wanazuoni wa Kiwahhabi wa zama zake kwamba Qur'ani Tukufu imepotolewa, amesema:
Lakini wale ambao, kwa kutaja Hadith kama hizo, wadhania kwamba nassi ya Qur'ani imepotolewa, bila shaka wanakosea.
(2) Abu Ja'far Muhammad b. Ali b. Baabawayh al-Qummi: Mwanachuoni huyu ni maarufu zaidi kwa jina la al-Shaykh as-Saduq na alifariki dunia katika mwaka 381 Hijriyyah. Yeye amesema hivi katika kitabu chake kiitwacho al-l'tiqaadaat:
lmani yetu ni kwamba Qur'ani ambayo Mwenyezi Mungu s.w.t. amemteremshia Mtume Wake Muhammad s.a.w.w, ni hii hii iliyo baina ya majalada mawili na iliyomo mikononi mwa watu; si zaidi ya hiyo... Na yeyote anayetusingizia kwamba twasema zaidi ya hivyo, basi huyo ni mwongo.
(3) Sayyid al-Murtadhaa Ali bin al-Husayn al-Muusawi al-Alawi: Huyu ni mwanachuoni mwingine mkubwa wa Kishia aliyefariki dunia katika mwaka 436 Hijiriyyah. Yeye, katika kujibu maswali ya Taraabulusiyyaat, amesema:
Ujuzi wa kwamba mapokezi ya Qur'ani ni sahihi ni kama ujuzi wa nchi na miji, matukio makubwa makubwa ya kihistoria, vitabu mashuhuri, na mashairi yaliyoandikwa na Waarabu. Hili ni kwa sababu hamu na sababu za kuinakili na kuihifadhi Qur'an zilishitadi na kufikia kiwango ambacho hakikufikiwa na hayo mengine tuliyoyataja.... katika zama za Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. Qu'rani ilikuwa ni mkusanyo uliotungamanishwa kama ulivyo hivi sasa. Mtume s.a.w.w. alikuwa hata ameteua masahaba wa kuihifadhi kwa moyo na kuilinda. Pia ilikuwa ni desturi (ya baadhi ya masahaba) kuisoma mbele zake ili kuhakikisha kuwa ndivyo. Kikundi cha masahaba, kama vile Abdullah b. Mas'ud, Ubayy b. Ka'b, na wengineo walikiihitimisha Qur'ani mbele za Mtume s.a.w.w. hitima kadha wa kadha. Na yote haya yaonyesha, hata kwa taamuli ndogo, kwamba Qur'ani ilikuwa ni mkusanyo uliopangwa; haukukatika kipande wala haukutawanyika.... Na kwamba yeyote katika Imamiyya (Shia Ithnaashari) au Hashwiyya (wasiokuwa Shia), anaye amini kinyume cha hivyo, basi kinyume hicho chatokana na watu wa Hadith walionakili Hadith dhaifu wakidhania ni sahihi; hali Hadith dhaifu kama hizo haziwezi kulirudi jambo ambalo usahihi wake unajulikana kwa njia isiyo na shaka.

Maneno hayo unaweza kuyaona katika Majma'ul Bayaan, Juzuu ya Kwanza, uk. 15.

Comments