Tukio hili la Mtume kwenda mbinguni
limethibitishwa na Mwenyezi Mungu katika kitabu chake kitukufu katika surah
mbili yaani Isra (sura ya 17) na Najm.
Katika Isra Allah anasema,
“sifa ni za Allah aliyemsafirisha mja wake kutoka Msikiti Mtakatifu Haram hadi
Mskiti wa Aqsa, palipobarikiwa ili kumwonesha alama na dalili zetu. Kwa hakika
Yeye ni msikivu na mwenye kuona”.
Kutokana
na aya hii,tunapata ushahidi kuwa Mtume (s.a.w.w) alisafiri mzima mzima na wala
sio ndoto kama baadhi ya watu wanavyodai. Lakini pia tunaona kuwa safari hii ni
ya kimiujiza ya mtu kusafiri toka Maka hadi Yerusalem na kurudi kwa usiku mmoja
tu. Japokuwa aya inaelezea safari ilianzia Maka na kuishia Yerusalem lakini ni
ukweli kuwa alipofika Yerusalem alipaa angani ili Allah akamuonesha ukubwa wa
uumbaji wake.
Katika Surat Najm utapata
maelezo mapana zaidi kuhusu safari hii tukufu.
Mtume (s.a.w.w) alipofika
aliwaambia Maquraish kuwa alimuona malaika Jibrail katika umbo lake halisi.
Maqraish walisimama na kuanza kumpinga. Allah analithibitisha hili kwa aya zifuatazo,
“mtampinga kwa kitu alichokiona? Kwa hakika alimuona (Jibrail) pembeni ya mti (mbingu
ya saba) jirani na Pepo. Wakati ambapo mti ulikuwa umefunikwa, macho ya (Muhammad)
hayakumdanganya. Kwa hakika aliona alama kuu kabisa za kuthibitisha uwepo wa Mwenyezi
Mungu. (soma Surat Najm)
Comments
Post a Comment