TUKIO LA ISRA NA MIRAJ; UTANGULIZI

Kuamini yasiyonekana ni sehemu muhimu katika Imani ya kiislamu. Mfano wa haya ni kumwamini Allah, kiama, Jahanam na pepo, malaika, majini, mitume, vitabu. Mambo yote haya kwa dhahiri tumeyaamini bila kuyaona.
Safari ya Usiku (Isra) ni sehemu hii ya kutakiwa kuamini tusiyoyaona kwa macho yetu na hiki kilikuwa kipimo cha kuipima imani ya waislamu wa awali. Wapo waliolikubali tukio hili na wapo waliolikataa katakata na kuacha kabisa Uislamu.
Tukio hili limeandikwa katika Qur’an na hadith na lina sehemu mbili. Sehemu ya kwanza ni kusafiri kutoka Maka hadi Yelusalem (Israa) na sehemu ya pili ni kutoka Yerusalem hadi mbinguni (miraj).
Mtume Mohammad (s.a.w.w) alianza safari akiwa na malaika Jibrail kutokea nyumba ya Umm Al-Hani dada wa Imam Ally (a.s) katika mji wa Maka kwa kumtumia mnyama aitwaye Buraq hadi msikiti wa baitil Aqsa ulioko Palestina ya sasa. Alipitia maeneo kadhaa kama vile Bayt al Laham (Bethlehemu), mahala alipozaliwa Nabii Issa (Yesu). Akiwa angani aliona umbile zima la ulimwengu na sayari na nyote zilizosheheni angani. Pia aliongea na malaika na roho za mitume waliomtangulia. Tena akiziona kwa karibu zaidi Pepo na moto wa Jahanam.
 Safari hii iliishia sehemu iitwayo Sidratul Muntaha, mahala patakatifu palipojaa nuru kila aina ya miujiza. Alirejea nyumbani kwa kupitia njia ile ile aliyoendea.
Wakati akirejea aliupita msafara wa kibiashara wa Makuraish ambao katika safari yao walimpoteza ngamia mmoja na wakiwa wanamtafuta. Mtume alikunywa maji waliyokuwa wamebeba watu hawa. Jua lilipochomoza alikuwa amekwisha fika pale pale nyumbani kwa Umm Hani.
Aliwakusanya Makuraish na kuwahadithia kuhusu safari yake hii. Habari hizo zilienea kwa kasi na kumfikia kila mtu katika eneo hilo. Makraish hawakuamini kabisa masimulizi haya ya Mtume
Makraish wakaanza kuulizana kuhusu ni nani anayejua vyema namna ulivyomsikiti wa Baitil Aqsa ili aulize Mtume (s.a.w.w) aeleze ukoje ili kuthibitisha kama alifika huko.

Alipoulizwa Mtume kufafanua msikiti ule ukoje, akaeleza vizuri sana na tena akaongeza kwa kuwaeleza tukio la msafara wao wa biashara na namna walivyokuwa wakimtafuta ngamia aliyepotea. 

Comments