BAHLUL NA CHAKULA CHA KHALIFA
Siku moja Harun al-Rashid alimpelekea Bahlul sinia iliyojaa kwa vyakula mbalimbali. Mfanyakazi alipomwakilishia Bahlul vyakula hivyo, alimwambia: "Hivi ni vyakula makhususi vya Khalifa na amekutumia wewe uvile." Bahlul alimtupia mbwa aliyekuwa ameketi karibu, vyakula vyote alivyoletewa.
Siku moja Harun al-Rashid alimpelekea Bahlul sinia iliyojaa kwa vyakula mbalimbali. Mfanyakazi alipomwakilishia Bahlul vyakula hivyo, alimwambia: "Hivi ni vyakula makhususi vya Khalifa na amekutumia wewe uvile." Bahlul alimtupia mbwa aliyekuwa ameketi karibu, vyakula vyote alivyoletewa.
Alipoyaona hayo, mfanyakazi wa Harun al-Rashid alighadhabika mno na kusema kuwa hiyo ilikuwa ni kumvunjia heshima Khalifa na angalimjulisha hivyo. Hapo Bahlul alimjibu: "Ewe kaa kimya! Iwapo na mbwa atafahamu kuwa vyakula hivyo vinatoka kwa Khalifa, naye pia ataacha kuvila!
Fundisho: Inatupasa kukatalia zawadi kutoka kwa waonevu na wadhalimu ili visituathiri sisi kutotimiza wajibu wetu wa ukweli na haki. TUSIMAME KWENYE HAKI DAIMA.
Comments
Post a Comment