BAHLUL NA MTUMWA ALIYEOGOPA MAJI

BAHLUL NA MTUMWA ALIYEOGOPA MAJI
Mfanya biashara mmoja alikuwa akisafiri katika jahazi pamoja na mtumwa wake kuelekea Basrah. Kwa bahati na Bahlul alikuwamo humo pamoja na watu wengineo. Mtumwa huyo alianza kulia palipotokea machafuko hapo majini. Wasafiri wote walikerwa na sauti za kilio cha mtumwa huyo.

Hapo Bahlul alimwomba ruhusa mfanyabiashara huyo ili atumie mbinu za kuweza kumkomesha mtumwa huyo, basi bila ya pingamizi alipewa ruhusa. Na hapo Bahlul alitoa amri ya kutupwa majini kwa utumwa na ilitekelezwa hivyo. Alipofikia wakati
wa kutaka kufa, alitolewa nje. Baada ya kutolewa nje, mtumwa huyo aliketi kimya akitulia katika kona moja ya jahazi.

Hapo baadaye, Bahlul alielezea: "Huyu mtumwa alikuwa haelewi raha na usalama wa jahazi inapokuwa majini. Pale alipotupwa majini ndipo alipotambua kuwa jahazi ni mahala pa raha
na usalama."

Fundisho:
1.  Amesema mtume (s.a.w.w.): "Safirini na mutajitajirisha (kwa uzoefu na uelewano)."
2.  Amani iliyopo nchini kwetu ni muhimu sana na hatuna budi kuilinda kwa juhudi zote. Endapo tutaichezea, amani ikitoweka tutajuta na itakuwa vigumu kuirejesha.

3.  Ukitaka kujua madhila ya vita waulize waliopigana vita (vita si lelemama).

Comments