Bahlul

Bahlul ni muislamu aliyekuwapo katika zama za Harun al-Rashid khalifa wa Mawahhabi. Bahlul alikuwa ni mmoja wa wanafunzi bora wa Imam Jaafer as-Sadiq (a.s.) na vile vile alikuwa mpenzi wa Ahli-Bayt (a.s.) wa Mtume (s.a.w.w.).
Vile vile inasemekana kuwa Bahlul alikuwa na undugu wa Harun Rashid kwa upande wa
mama yake na riwaya nyingine imesemwa kuwa alikuwa jamaa wa karibu wa Harun.
Qadhi Nurallah Shushtary anasema katika kitabu chake Majalis al-Muuminin Bahlul alikuwa
ni mtu mwenye akili mno ambaye kwa sababu fulani fulani alijegeuza mwendawazimu.

Bahlul alizaliwa Kufa na jina lake la asili lilikuwa Wahab bin Umru. Kwa mujibu wa riwaya
moja, Harun Rashid alimwona Imam Musa bin Jaafer (a.s.) kama tishio kubwa kwa kubakia
utawala wake. Hivyo alijishughulisha katika mbinu za kutaka kumwua. Na aliweza kutafuta
hila moja ya kumwua. Hivyo alimzulia dai la kuasi na hivyo aliwataka hukumu Maulamaa
ya kumwua Imam, ambamo Bahlul pia alikuwamo. Wote walitoa fatwa ya kuuawa kwa
Imam (a.s.) lakini Bahlul aliipinga. Bahlul alimwendea Imam (a.s.) na kumjulisha yale
yaliyokuwa yakitokea, na alimwambia Imam (a.s.) ampatie ushauri na njia za kuyakabili
hayo. Imam a.s. alimwambia kuwa ajigeuze na awe mwenda wazimu. Vinginevyo na yeye angeuawa kama imam.

Hii ndiyo sababu ya yeye kuwa mwenda wazimu kwa matakwa ya Imam (a.s.) na hivyo
aliweza kuepukana na adhabu na maangamizi ya Harun Rashid, aliyekuwa Khalifa wakati
huo. Na hivyo bila ya woga wowote akijifanya mwenda wazimu, aliweza kukabili, kumsuta
hata Khalifa na mawaziri wake na papo hapo aliwatetea wanyonge na wale wote waliokuwa
wamedhulumiwa. Pamoja na hali yake hiyo, watu walimpenda kwa mioyo yao, hadi leo
hekaya zake zinasimuliwa katika vikao na kujifunza mengi kutokana hayo.

Kwa mujibu wa riwaya ya pili - ambayo inasadikiwa zaidi. Masahaba na wapenzi wa Imam
(a.s.) walikuwa wametingwa na udhalimu wa Khalifa na watawala wanzake. Hivyo wote
walimwomba Imam (a.s.) uongozi kuhusu swala hilo. Imam (a.s.) aliwajibu kila mmoja kwa
herufi moja tu. "Jim" kwa hivyo walielewa kuwa hapakuwapo na haja ya kuulizia ziada.
Kila mmoja alielewa hio herufi tofauti tofauti. Mmoja alielewa "Jila Watan" yaani kutoka
nyumbani, mwingine alielewa 'Jabl yaani 'Mlimani' na Bahlul alielewa kuwa ikimaanisha
'Junuun' Yaani "Uenda wazimu" na hivyo alijigeuza hivyo na kwa hayo, wote waliweza
kunusurika na janga hilo la kuteketezwa na udhalimu wa Khalifa.
Bahlul alikuwa akiishi maisha ya starehe na bora kabisa lakini baada ya ishara hiyo ya
Imam (a.s.) aligeuzia uso dunia na kuziacha starehe zote hivyo akaishi maisha ya utawa na
akawa na mavazi yaliyokuwa yamechakaa. Yeye alipendelea kuishi uwanjani kuliko
majumba ya Wafalme, vile vile aliishi kwa kipande kikavu cha mkate kuliko kutegemea
misaada ya hisani ya Khalifa kwani alikuwa akijiona yu bora kuliko Khalifa Harun Rashid,
mawaziri wake na Baraza lake zima.

Bahlul kwa hakika, alikuwa mcha Mungu na mpenzi wake, mwenye akili sawa na Aslim
kamili. Yeye alikuwa ni mtu mwenye akili sana na fahamu zaidi na mwenye kutoa majibu ya
papo hapo na mtatuzi wa masuala katika zama zake. Jina lake halikuwa mashuhuri tu
miongoni mwa watu wenye akili tu bali kwa amri ya Imam (a.s.) alijifanya mwenda wazimu
na hivyo aliweza kuhifadhi Din na Sharia na kuelezea uhakika na ukweli wa Ahli Bayt (a.s.).

Katika zama hizo hapakuwapo na njia nyyingine ila yeye kujifanya mwenda wazimu
amasivyo Harun Rashid angalimwua. Kama vile Harun Rashid alisikiliza uthibitisho wa
Uimam wa Musa ibn Jaafer (a.s.) kutoka mwanafunzi mmoja wa Imam Jaafer as-Sadiq (a.s.)
Hisham bin Hikam, na akamwambia Waziri wake Yahya ibn Khalid Barki: "Ewe Yahya!
Maneno ya mtu huyu, Hisham, kwangu mimi ni sawa na tishio la mapanga laki moja, lakini
jambo la kushangaza ni kule kubainika kwake hai wakati mimi natawala!"
Harun alibuni kila aina ya mbinu za kutaka kumwua Hisham. Na alipopata habari hizo,
alitorokea Kufa ambako aliishi nyumbani (mafichoni) mwa rafiki yake, na katika kipindi
kifupi alifariki.

Nitakuwa nikileta visa na habari kutoka katika maisha ya Mshia huyu Mashuhuri wa zama zake. 

Comments