Tunaelewa vizuri kwamba makusudi ya
kuumbwa kwetu ni kutupatia kufikia ukamilifu wa roho. Na kwa ajili ya kutimiza
makusudi hiyo roho kuelekea upande wa juu kiutakatifu; vile vile inapasa roho
iangalie utaratibu na usalama wa kiwiliwili. Anapokuwa mtu yu macho, tena mandhali
tumbo lake limejaa, basi roho haijaliwi kupata wasaa kuelekea upande wa Mola
kwa vile umeshughulika na mambo ya mwili; inaziwika kuipata shabaha ya kuumbiwa
kwake.
Kwa hivyo mtu akifunga mchana kiwiliwili
kinakuwa chepesi, na tukifanya mazowea usiku pia tule chakula chepesi na kiasi
cha dharura tu, hapo roho itapata wasaa na faragha kwa upesi. Ijapokuwa kwa
muda huo mdogo wa mwezi mmoja mfululizo bila ya taabu itaweza kushikamana
uhusiano wake wa juu kwa furaha na kupata daraja tukufu za akhera.
Uvivu unapopungua itumie fursa hii kufanya
ibada mbali mbali, kama vile kuswali na kutoa sadaka. Ibada hizi zina faida
kubwa kwa mwanadamu na zitapelekea kuwa kipenzi wa Mwenyezi Mungu. Malipo yake
ni makubwa kiasi kwamba ni Allah peke yake ndiye anayefahamu.
Comments
Post a Comment