kiwiliwili cha binadamu ni kama mashine
ambayo huhitajia mapumziko kidogo. Na mapumziko hayo hayawezi kupatikana hadi
mtu ajizuie kula na kunywa kwa muda ambao ala ya kuyeyusha chakula (tumbo)
itulie. Vile vile upatie moyo na vifaa vyote vya ndani mapumziko na kujisafisha
vyenyewe. Basi kwa kufunga saumu hupungua, na pengine hutoka kabisa maradhi.
Elimu ya afya siku hizi imethibitisha
kwamba mtu kuweka siha yake vizuri, inampasa kwa uchache afunge saumu, siku
moja katika kila wiki, au wiki moja kila mwezi na bora mwezi mmoja kila mwaka.
Vile vile imethibitisha elimu za sasa
kwamba bidii za akili na nguvu ya mwili huzidi kwa kuuweka mwili katika hali ya
njaa. Bila shaka faida na maendeleo yanaweza kupatikana kwa kufunga saumu,
kuliko mtu anapokuwa amejaa tumbo na uvivu pia umemshika. Madaktari na matabibu
katika maradhi mara nyingi huwaongoza wagonjwa wao kufunga. Yapo baadhi ya
maradhi kama mtu akifunga saumu tu badala ya kutumia dawa atapona kabisa.
Baada ya kujua na kufahamu hayo yote, basi
tutapata hakika kuwa Mwenyezi Mungu kwa njia na taratibu bora kabisa
ametuamrisha kuacha kula; na kitendo hicho kakifanya kuwa ni Ibada. Hii ni
uthibitisho dhahiri wa huruma juu ya viumbe wake, isitoshe kakifanya hicho
kitendo (kufunga) si faida ya duniani tu, bali kwa akhera pia. Juu ya hayo yote
ikiwa tutahalifu, tutakuwa watu wajinga mno, tusio na mfano kwa kuzisahau
hisani zake.
Si vibaya hapa tukisema kwamba baada ya
kujua faida ya saumu kwa kiwiliwili, basi mtu haifai kwake ukifika usiku ale
chakula kwa wingi kulipia njaa ya mchana, au kula vitu ambavyo ni vizito kwa
tumbo na vyaweza kumletea taabu na maradhi. Kwa hiyo ni bora sana kutumia
chakula chepesi anapofuturu ili apate faida kwa kiwiliwili na
roho
Comments
Post a Comment