HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU

Uislamu una mfumo mzuri wa ndoa na haki za wanawake, kinyume na wanavyoamini watu wa Magharibi na wengine waliokuwa na kasumba ya umagharibi.
Inakubaliwa na kila rafiki na adui kuwa Qur.ani Tukufu ilifufua haki za wanawake. Hata maadui wanakiri angalau kwamba Qur’ani wakati wa kuteremshwa kwake ilichukuwa hatua kubwa katika kuboresha hali ya mwanamke na kurejesha haki zake za binadamu.
Qur.ani ilifufua haki za mwanamke kama mwanadamu na kama mwenzi wa mwanaume katika utu na haki za binadamu lakini haikupuuza jinsia yake wala jinsia ya mwanaume. Kwa maneno mengine Qur.ani haikupuuza maumbile ya mwanamke.

Ndio maana kuna kuwafikiana kikamilifu kati ya kanuni za
maumbile na kanuni za Qur.ani. Mwanamke katika Qur.ani ni sawa na mwanaume katika maumbile. Vitabu hivi viwili vikubwa vya kimungu (Qur.ani na maumbile), kimoja kikiwa kimeumbwa na kingine kikiwa kimekusanywa, vinakubaliana na kuafikiana kabisa. Nia ya kitabu hiki ni kuangazia na kuelezea kuafikiana huku.

Kutokana na umuhimu wa maudhui hii nitaendelea kutoa makala katika maudhui hii kwa sababu makala hizi zitawanufaisha wengi, waislamu na wasio kuwa waislamu.

Comments