Hedhi ni damu inayomtoka mwanamke katika utupu wa mbele,
aliyefikia miaka tisa. Na mwisho wa kutoka kwa damu ni miaka hamsini.
Inazuiwa
kwa mwenye hedhi mambo yafuatayo:
(a)
Kushika Qur-an, (b) Kukaa Msikitini, (c) Kuswali, (d) Kufunga saumu, (e)
Kumwingilia, (f) Kumwacha (kumpa talaka).
Muda
wa hedhi ni siku tatu kwa desturi, na wingi wake ni siku kumi. Mwenye hedhi
baada ya kutoharika anapaswa kulipa funga na wala hatalipa swala. Nifasi ni,
damu ambayo hutemwa na mfuko wa uzazi kwa sababu ya kuzaa. Kwa hiyo, mwenye
mimba akizaa na kusitoke damu, basi hakuna josho, muda wa nifasi ni siku kumi.
Inazuiwa
kwa mwenye nifasi mambo yaleyale yanayomzuia mwenye hedhi. Je, vitabu vya
wakristo vinasema nini katika rnada hii? Na tusome;
"Mwanamke
yeyote anapokuwa mwezini, atakuwa najisi kwa muda wa siku saba. Mtu yeyote
atakayemgusa mwanamke huyo atakuwa najisi mpaka jioni. Kitu chochote
anacholalia au kukalia wakati yu najisi kitakuwa najisi. Mtu yeyote atakayegusa
Kitanda cha huyo mwanamke ni lazima ayafue mavazi yake na kuoga kwa maji, naye
atakuwa najisi mpaka jioni. Mtu yeyote atakayegusa kitu chochote anachokalia
mwanamke huyo ni lazima ayafue mavazi yake na kuoga kwa maji, naye atakuwa
najisi mpaka jioni." Mambo ya Walawi 15:19-22.
Ukristo
unamnyanyapaa mwanamke katika siku saba anazokuwemo katika hedhi. Lakini, si
yeye peke yake bali kila mtu sasa anayegusa chochote kilichoguswa na mwanamke
huyo, naye huwa najisi, inamlazimu kufua mavazi yake na kuoga, hata hivyo
huendelea kuwa najisi mpaka jioni'
Comments
Post a Comment