ITIKADI YA SHIA ITHNA ASHARIA KUHUSU KUWEPO KWA MOLA MTAKATIFU.

ITIKADI YA SHIA ITHNA ASHARIA KUHUSU KUWEPO KWA MOLA MTAKATIFU.
Sisi tunaamini kuwa Mwenyeezi Mungu ndiye muumbaji wa vitu vyote, na athari ya utukufu na elimu yake inaonekana kwa uwazi kabisa katika kila kiumbe ulimwenguni, katika umbile la mwanaadamu, wanyama, mimea, katika nyota ziliopo mbinguni, na katika kila kitu ulimwenguni.
Sisi tuna itikadi ya kuwa; kila tukifikiri na kutafakuri zaidi kuhusiana na siri ya viumbe vyote duniani, tutafahamu utukufu wa elimu na qudra ya dhati ya Mola Mtakatifu, na kwa kuonekana maendeleo ya elimu na taaluma ya wanaadamu ya kila siku kunapatikana na kufunguka elimu mpya kutokana na elimu na hekima zake Allah (s.w), na tafakuri za wanaadamu zinazidi kukua na kuenea kwa wingi zaidi, na tafakuri hizo ndio chanzo cha kuwa karibu naye Mola mtakatifu na kunufaika na upeo wa nuru ya utukufu wake. Qur-ani takatifu inasema:-
Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini. Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni?.2
Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi na kukhitalifiana usiku na mchana ziko Ishara kwa wenye akili. Ambao humkumbuka Mwenyezi Mungu wakiwa wima na wakikaa kitako na wakilala, na hufikiri kuumbwa mbingu na ardhi, wakisema: Mola wetu Mlezi! Hukuviumba hivi bure. Subhanaka, Umetakasika! Basi tukinge na adhabu ya Moto.3

Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tumemsikia mwenye kuita akiitia Imani kwamba: Muaminini Mola wenu Mlezi; nasi tukaamini. Basi tusamehe madhambi yetu, na utufutie makosa yetu, na utufishe pamoja na watu wema.1


REJEA:
[1] Surat Al-Imrani Aya ya 193
[2] Surat Adh-Dhariyat Aya ya 20-21

[3] Surat al-Imrani Aya ya 190-191

Comments