JINSI KABURI LA AMIRU’L-MU’MININ ALI (A.S.) LILIVYOGUNDULIWA.

kaburi la Amiru’l-Mu’minin ‘Ali (as) liligunduliwa miaka 150 baada ya kifo chake kutokana na kufichwa na Ahlulbayt (a.s) ili maadui wa Mtume na Ahlulbayt isijekujua alipozikwa na hivyo kulidhihaki kaburi hilo na hata kumfukua na kumuwamba msalabani.
Uonevu wa Banu Umayya ulikuwa mkali sana wakati wa mwisho
wa uhai wa ‘Ali, hivyo aliagiza katika wosia wake kwamba azikwe kwa siri wakati wa usiku, na kwamba isiachwe alama yoyote ya kaburi hilo.
Ni jamaa zake wachache tu wa karibu na watoto wake ndio waliohudhuria mazishi yake. Asubuhi ya tarehe 21 Ramadhan siku ambayo ilikuwa ndio azikwe, misafara miwili ilitayarishwa. Mmoja ulielekezwa kwenda Makka, na mwingine kwenda Madina.
Hii ndio sababu iliyofanya kwa miaka mingi kaburi lake lisijulikane, isipokuwa kwa jamaa zake wachache na watoto wake tu. Na wengi wa Masunni waliamini kuwa jeneza la imam Ally (a.s) lilipaa kwenda mbinguni kutokana na kukosa kwao kujua imam alizikwa wapi.
Mwenendo wa Banu Umayya uliokuwa sio wa kidini, Walikuwa maadui makhususi wa jamaa ya kizazi cha Mtukufu Mtume (s.a.w.w). Wangeweza kulivunjia heshima kaburi lake. Subuhana-LLAH! Maovu yalioje waliyoyafanya! Damu iliyoje waliyoimwaga, na heshima zilizoje walizozivunja!
Kwa aibu kubwa, wanachuoni wa kisunni wakubwa wameandika jinai zao nyingi. Allama Maqrizi Abu’l-Abbas Ahmad bin Ali Shafi’i ameandika maovu ya Banu Umayya yanayoumiza moyo kabisa katika kitabu chake Annaza’ Wa’t-takhasum fima baina Bani Hashim wa Bani Umayya.

Hakika kimeweka wazi maovu makubwa sana kwa mfano mwaka wa pili wa utawala wa Yazid bin Muawiyya (khalifa wa kiwahabi) waliuteka mji wa Makkah na kuwa waislamu elfu saba na kuwabaka wanawake elfu tatu tena kwa amri ya khalifa huyu wa Mawahhabi pale alipowaambia kuwa kila kitu ndani ya mji wa Maka ni halali kwao yaani wafanye watakavyo. 

Comments