Nimeonelea niandae mada kwa ajili ya
kuuelimisha Umma wa Kiislamu katika Afrika Mashariki kuhusu kundi balaa
ninaloitwa takfir. Takfir ni msamiati ambao unawakilisha makundi yote
yanayojidai kuwa ni ya kiislamu na huku kazi yao ni kuwakufurisha waislamu
wenzao na kuhalalisha mauaji dhidi yao.
Takfir wameendesha matukio ya kigaidi maeneo
mengi duniani kwa kisingizio cha kwamba hao wanaowauwa ni makafiri au washirikina.
Kutokana na uvivu wa kusoma wa watu hawa wamekuwa wakimwona mtu akifanya jambo
lolote wasiololizoea basi humwita mtu huyo kafiri na kuhalalisha kumuua mtu
huyo mara moja.
Hii imenisababisha nimkumbuke mwalimu wangu
wa Sociology wakati nilipokuwa chuoni ambaye aliwahi kutuambia kuwa ukimwona
mtu akimdhalau mtu mwingine elewa wazi mtu huyo anayemdhalau mwenzake hakusoma
tamaduni za wenzake. Hivyo kutokana na kukosa kwake maarifa anaamua kumdhalau
na kumdhalilisha mwenziwe. Lakini ukweli ni kuwa mtu huyo akipata wasaa wa
kukaa na kujifunza utamaduni wa mdharauliwa atakuja kugundua kuwa yule
aliyekuwa akimdhalau ni bora kuliko hata yeye mwenyewe.
Kwa hiyo asili ya utakifiri ni ujinga (murrakab)
wa watu hawa ambao utawakuta wamekimbilia kufanya ibada lakini bila kutafuta
elimu ya kile anachokiabudu ili akiabudu kwa ufasaha.
Ndipo wakipata hoja kutoka kwa mashia utawasikia
wakisema, hao ni makafiri kwa sababu wanayo elimu kubwa sana lakini wanaitumia
vibaya, kupotosha watu. Ukiwaambia twende ukajadiliane nao, hukataa kwa kuwa
anayo yaamini hana yakini nayo wala ushahidi ya kuyathibitisha.
Ninahakika kuwa hayo niliyoyaandika yanatoka
kuarifisha maana ya takfir na kwa msingi huu wasomaji wangu wamewaelewa takfiri
wote na makundi yao hapa Afrika Mashariki. Labda kwa ufupi, ukimsikia mtu
anamwita mtu mwingine kafir huyu basi elewa kuwa huyo ni takfir na yumo katika
kundi potofu.
Imepokelewa na Kahhak kuwa Mtume wa Allah (s.a.w.w)
alisema, “yeyote atakaye mlaani muumini, ni kana kwamba amemuua muumini huyo.
Na yeyote atakaye msingizia muumini kuwa ni kafir, itakuwa kana kwamba amemuua
pia”.
Hadith hii imepokelewa na Imam Bukhari na
inaaminiwa na waislamu kuwa ni sahihi.
Abdullah bin Umar (r.a) alisema kuwa Mtume (s.a.w.w) alisema, “yeyote atakaye mwita ndugu ewe kafir,
itakuwa mmoja wao ni kafir kweli.
Hadith zote hizo mbili zimepokelewa na Imams, Ahamad, Bazzar, Tabaraan,
Baihaqi na kuandikwa katika vitabu: Majma’uz-Zawaa’id na Musnad Abu ‘Awaanah.
Mada
hii itaendelea ili kuwaonya ndugu zangu waislamu na wajiepushe na kundi hili la
shetani. Siwataji kwa majina kwa sababu wanaeleweka. Hata mada hii wakiisoma
utakuta wananihukumu niuawe au kuniita kafir au yote mawili.
Comments
Post a Comment