KISA CHA KUADHIBIWA NA
ALLAH WALIOPINGA UKHALIFA WA IMAM ALLY WALIADHIBIWA
Baada ya imam Ally (a.s)
kutangazwa na Mtume (s.a.w.w) kuwa khalifa wake wa kwanza katika Hija ya kuaga
na maeneo Ghadir Khum, kuna watu walijitokeza kulipinga hilo kama wanavyo fanya
mawahhabi na masalafiya leo hii. baada ya kuenea kwa habari za Ghadir Khum na
kusimikwa kwa Imam Ali kuwa ni Khalifa wa Waislamu kutokana na kauli ya Mtume
alipowaambia "Aliyeshuhudia tukio hilo amfikishie habari asiyehudhuria
".
Habari hizo za tukio la
Ghadir zilimfikia Harith bin Nuuman Al-Fihri na hakufurahishwa na habari hizo-
Hapa kuna dalili kwamba walikuwepo watu waliodai kuwa ni Masahaba wakiishi
Madina ambao walikuwa wakimchukia Ali na pia Mtume (s.a.w.w). Basi huyu bwana
alimsimamisha mnyama wake mbele ya mlango wa msikiti akaingia kwa Mtume
(s.a.w.w) akasema: "Ewe Muhammad bila shaka wewe umetuamuru tushuhudie
kuwa hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu na kwamba wewe ni Mtume wa Mwenyezi
Mungu, tumekukubalia hilo, na umetuamuru tusali mara tano kwa siku, tufunge
Ramadhan, Tuhiji na tutoe zaka mali zetu tukakukubalia, kisha hukuridhika kwa
haya mpaka umeinyanyua mikono ya mwana wa ammi yako na umemboresha juu ya watu
ukasema:
"Yeyote ambaye mimi
ni mtawalia mambo yake basi Ali ni mtawalia mambo yake". Jambo hili latoka
kwako au latoka kwa Mwenyezi Mungu"?
Mtume wa Mwenyezi Mungu
akasema hali ya kuwa macho yake yamekuwa mekundu: "Namuapa Mwenyezi Mungu
ambaye hapana Mola isipokuwa yeye, jambo hilo latoka kwa Mwenyezi
Mungu na halitoki kwangu" Akasema maneno hayo mara tatu.!!
Harith alisimama huku
akisema: "Ewe Mwenyezi Mungu ikiwa ayasemayo Muhammad ni ya kweli, basi
tuletee mawe toka mbinguni au utuletee adhabu kali".
Msimulizi wa kisa hiki
anasema: "Wallahi hakumfikia ngamia wake bali Mwenyezi Mungu alimpiga kwa
jiwe toka mbinguni likaangukia kichwani na kutokea kwenye makalio, akafa. Pale
pale Mwenyezi Mungu akateremsha aya hii isemayo:-
"Muombaji
aliomba adhabu itakayotokea (adhabu ambayo) haina wa kuizuia kwa
makafiri."
Tukio hili wameliandika
wanachuoni wengi wa Kisunni wasiokuwa wale tuliokwisha kuwataja,
basi mwenye kutaka ziyada kutoka katika rejea ni juu yake kutazama kitabu
kiitwacho Al-Ghadir cha Al-Allamah Al-Amin.
REJEA
[1] Maarij, aya 1-2
[2] Ibnu Qutaibah,
ndani ya kitabu kiitwacho Al-Maarif uk. 251
[3] Imam Ahmad bin
Hambal ndani ya Musnad yake Juz. 1 uk.119
Comments
Post a Comment