Imeandikwa
katika vitabu vya hadithi vya Kisunni kwamba Mtume alizoea kuswali Swala zake
kwa kuzitenganisha na halikadhalika kwa kuzichanganya akiwa nyumbani na bila
kikwazo chochote. Hadithi nyingi zinathibitisha ukweli huu. Muslim Bin Hajjaj
katika Sahih yake,
katika mlango wa “Jam’a Baina’s-Salatain fi’l-Hadhar,” anasema kwamba Ibn Abbas
alisema: “Mtume alizoea kuswali Swala ya Dhuhr na Alasir kwa kuziunganisha na
halikadhalika hivyo hivyo kwa Swala za Magharib na Isha bila ya kuwa na kikwazo
cha kufanya hivyo, au wakati alipokuwa nyumbani.”
Tena
Ibn Abbas alisimulia: “Tuliswali rakaa nane za Dhuhr na Alasir na baadaye rakaa
saba za Magharib na Isha kwa kuziunganisha tukiwa pamoja na Mtume.”
Hadithi
hiyo hiyo imesimuliwa na Imamu Ahmad Bin Hambal katika Musnad yake jalada la kwanza, ukurasa wa 221. Halikadhalika, Imamu Muslim
ananukuu idadi ya hadithi kuhusiana na suala hili. Anamnukuu Abdullah Bin
Shaqiq akiwa amesema kwamba siku moja Abdullah Ibn Abbas alikuwa anahutubia
baada ya Swala ya Alasir mpaka jua likazama na nyota zikawa zinaonekana. Watu
wakapiga makelele, “Swala, Swala,” lakini Ibn Abbas hakuwajali. Kisha mtu mmoja
wa Bani Tamimi alipiga kelele, “Swala, Swala.” Ibn Abbas akasema: “Unanikumbusha
mimi kuhusu Sunna, lakini mimi mwenyewe nimemuona Mtume akikusanya Swala za Dhuhr
na Alasir halikadhalika Magharib na Isha.” Abdullah Bin Shaqiq
alisema
alikuwa hana hakika kuhusu maneno haya na alikwenda kwa Abu Huraira kumuuliza
kuhusu maneno hayo. Alithibitisha kile alichokisema Ibn Abbas.
Kupitia
sanad nyingine ya wasimuliaji, Abdullah Bin Shaqiq alisimulia kutoka kwa Aqil kwamba
siku moja Abdullah Ibn Abbas aliwahutubia watu juu ya mimbari. Alibaki pale kwa
muda mrefu mpaka giza likaingia. Wakati mtu mmoja alipopiga kelele mara tatu,
“Swala, Swala, Swala,” Abdullah Ibn Abbas alikasirika na akasema: “Ulaaniwe
wewe. Unathubutu kunikumbusha mimi kuhusu Swala, ingawaje wakati wa Mtukufu
Mtume tulizoea kukusanya Swala za Adhuhr na Alasir na halikadhalika Magharib
pamoja na Isha.”
Zarqani
katika Sharhe Mawatta cha Imamu
Malik, jalada la 1, katika sura ya Jama’a Baina’s-Salatain, ukurasa wa 263,
anaeleza, “Nisa’i alisimulia kutoka kwa Amru Bin Haram kutoka kwa Abi Sha’atha
kwamba Ibn Abbas aliswali Dhuhr na Alasir na halikadhalika Magharib na Isha kwa
pamoja mjini Basra bila kukawia au kitendo chochote kati yao. Alisema kwamba
Mtukufu
Mtume (s.a.w.w.) aliswali katika njia hii hii.”
Vile
vile Muslim katika Sahih yake na
Malik katika Mawatta, sura ya
Jam’a Baina’s- Salatain, na Imamu Hambal katika Musnad wanamnukuu Ibn Abbas kutoka kwa Sa’id Bin Jabir kwamba Mtukufu
Mtume (s.a.w.w.) aliswali Swala zake za Dhuhr na Alasir pamoja mjini Madina
bila kulazimishwa kufanya hivyo kwa hofu au hali mbaya ya hewa. Abu Zubair akasema
alimuuliza Abu Sa’id kwa nini Mtume alikusanya Swala hizo mbili. Sa’id akasema yeye
vile vile alimuuliza Ibn Abbas swali kama hilo hilo. Ibn Abbas alijibu kwamba
alikusanya Swala hizo mbili ili kwamba wafuasi wake wasije wakawekwa katika
uzito na shida zisizo na sababu.
Vile
vile, katika hadithi nyingine nyingi,
Ibn
Abbas inasimuliwa kwamba alisema Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wa Uislamu alikusanya
Swala za Dhur na Alasir halikadhalika na Magharib na Isha bila kulazimishwa
kufanya hivyo.
Kwa
sababu hii hakuna ulazima wa waislamu kuacha shughuli zao mara kwa mara na
kwenda msikiti kuswali bali wameruhusiwa kwenda msitini kuswali mara tatu kwa
siku ni hivi ndivyo Qur’an inavyosema, ya kuwa nyakati za swala ni tatu
japokuwa swala ni tano. Jua linageuka mchana, jua linapozama na subhi basi. Wale
wachapakazi ungana na sisi Mashia katika utekelezaji wa ibada kikazi kazi na
kuwahi kazi zetu mara moja. Hata hivyo mida wanayoswali masuni haina makosa kwa
sababu ni ndani ya mida ya kisheria.
Comments
Post a Comment