Kwa
desturi viongozi wa bani Umaya walikuwa wakiwawamba msalabani watu waliowaona
kuwa ni wapinzani wao. Na hata akifa mpinzani walikuwa wakiifukua maiti yake na
kuitundika na kusambukia msalabani.
Kwa
kuzingatia maovu ya ufalme huu uliolaaniwa, mwili wa Amiru’l-Muminin, ‘Ali (as)
ulizikwa wakati wa usiku, na hakuna alama ya kaburi hilo iliyoachwa. Kaburi
likabakia bila kuonekana mpaka wakati wa Khalifa Harun ar-Rashid. Siku moja
Harun alikwenda kuwinda katika eneo la Najaf, ambako paa waliishi kwa wingi.
Wakati
mbwa walipofukuza paa, walichukua hifadhi juu ya kilima kidogo (kilichotutumka
juu ya ardhi) cha Najaf, kilima ambacho mbwa hao hawakuweza kukipanda.
Mara
nyingi wakati mbwa waliporudi nyuma, paa waliteremka chini, lakini wakati mbwa wanapowarukia
tena, wale paa huchukua tena hifadhi juu ya kile kilima.
Harun
akatuma watu wake kwenda Najaf kuuliza. Walimleta mzee mmoja kwake na Khalifa
akauliza kuhusu siri ya kwa nini mbwa hawakupanda juu kilima.
Kugunduliwa Kwa Kaburi Tukufu La Ali.
Yule
Mzee akajibu kwamba anaielewa Siri yake, lakini alikuwa anaogopa kuitoa. Khalifa
akamhakikishia usalama wake, na yule mzee akamwambia: Siku moja nilikuja hapa
pamoja na baba yangu, ambaye alipanda juu ya kilima na akaswali pale.
Nilipomwuuliza
kuna nini pale, akasema kwamba waliwahi kuja pale na Imam Ja’far Sadiq kwa
ajili ya Ziara. Imam alisema kwamba hili ni kaburi Tukufu la Mheshimiwa babu
yake, Amur’l Mu’miniina Ali, na kwamba muda mfupi litakujajulikana.”
Kwa
amri ya Khalifa sehemu ile ilichimbuliwa, na alama za kaburi zikaonekana wazi
pamoja na ubao wenye maandishi ya Ki-Syria yenye maana; “Kwa jina la Allah,
Mwenye rehema, Mwenye kurehemu. Kaburi hili limetayarishwa na Mtume Nuh kwa
ajili ya Ali, wasii wa Muhammad miaka 700 kabla ya gharika.”
Khalifa
Harun alitoa heshima zake kwenye sehemu ile na akaamuru ule udongo urudishwe. Kisha
akasali rakaa mbili. Alilia sana na akajilaza juu ya kaburi. Baadae, kwa amri
yake, taarifa ya tukio lote ilitolewa kwa Imam Musa Kadhim huko Madina. Imam
alithibitisha kwamba kaburi hilo ni la Mheshimiwa babu yake, Amiru’l-Mu’minin
Ali, lipo mahala hapo.
Kisha
Harun akaamuru jengo la mawe lijengwe juu ya kaburi tukufu la Amiru’l-Mu’minin,
ambalo lilikuja kujulikana kama “Hajar Harun.” Kwa wakati huo habari zilisambaa
na Waislamu wakaizuru sehemu hiyo tukufu.
Huu
ni ushahidi kuwa Bani Umaya na mawahhabi wanapinga uongozi wa Imam Ally (a.s)
kwa sababu ya tamaa na hiyana, lakini nafsi zinawasuta kuwa hakuwahi kuwepo Mtu
bora Kama Imam Ally, baada ya Mtume (s.a.w.w). Kama isingekuwa hivyo kwanini
akalijengee kaburi la Imam Ally badala ya Mawiyyah au Uthuman?
Lakini
vile vile wanaopinga kujengea makuburi wamezua bida’a ambayo hata viongozi wao
wakifufuka watawashangaa.
Na mwisho
kuswali maeneo yenye makaburi sio kuyaabudu kama wanavyodanganya mawahhabi na
masalafi vinginevyo wakubali kuwa hata viongozi wao walikuwa washirikina.
Comments
Post a Comment