1-FUNGA:
Amesema
Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w): (Mwenye kufunga siku ya Jumatatu na
Alkhamisi ya mwezi wa Shaaban, Mwenyezi Mungu mtukufu atamuwekea fungu lake, na
mwenye kufunga siku ya Jumatatu na Al-khamisi ya mwezi wa Shaaban atakidhiwa
haja ishirini katika haja za kidunia, na haja ishirini kati ya haja za Akhera [6].
Na
imepokelewa kutoka kwa Amiril-muuminiin Ally (a.s) ya kuwa amesema: Amesema
Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w): (Kila Al-khamisi ya mwezi wa Shaaban mbingu
hupambika, na malaika husema ewe Mola wetu msamehe mfungaji wa mwezi huu, na
wajibu dua zao (hadi akafikia kusema) na mwenye kufunga kwenye mwezi huu siku
moja Mwenyezi Mungu huuharamisha mwili wake kuingia Motoni) [7].
Na
amesema kiongozi wetu Amiril-muminiin Ally (a.s): (Mwenye kufunga mwezi wa
Shaaban kutokana na mapenzi yake kwa Mtume (s.a.w.w) na kwa ajili ya
kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu alie takasika basi Mwenyezi Mungu atampenda na
kumkaribisha kwenye ukarimu wake siku ya kiama na atamuwajibishia pepo ) [9].
Na Imamu
wetu Abu Jaafar Al-baaqir (a.s) akasema: (Hakika funga ya mwezi wa Shaaban ni
funga ya manabii, na ni funga ya wafuasi wa mitume, basi mwenye kufunga mwezi
wa shaaban kwa hakika atakuwa amefikiwa na wito wa Mtume wa Mwenyezi Mungu
(s.a.w.w) kutokana na kauli yake, Mwenyezi Mungu amrehemu mwenye kunisaidia juu
ya mwezi wangu huu) [10].
Na Abu
Abdillahi As-swadiq (a.s) akasema: (Mwenye kufunga siku moja ya mwezi wa
Shaaban ataingia peponi) na (Mwenye kufunga siku tatu katika mwezi wa Shaaban
atawajibikiwa na pepo, na Mtume (s.a.w.w) atakuwa muombezi wake siku ya kiama) [11].
Na
imekuja kutoka kwa Hasan bin Ali bin Shuubah Al-harraniy katika kitabu chake
(Tuhaful-ukuul) kutoka kwa (Imam Ridhaa (a.s) katika barua yake kuelekea kwa
Maamun amesema: (Na funga ya mwezi wa Shaaban ni jambo njema nayo ni sunna)
([12]).
2-
KUFANYA ISTIGHFARI
Hilo
litatimia kwa kusema kila siku mara sabini: (Astaghfiru llah
wa’as’aluhut-tawbah) na (Astaghfirullah alladhi laa ilaha illa
huwar-rahmanir-rahiim, al-hayyil-qayyum wa atuubu ilaihi).
Na
tunafaidika kutoka kwenye habari hii kuwa dua na nyuradi zilizo kuwa bora
zaidi katika mwezi huu mtukufu ni kuomba istighfari.
Amesema
Imamu Ridhaa (a.s): (Mwenye kumuomba Mwenyezi Mungu istighfari katika mwezi wa
Shaaban mara sabini, Mwenyezi Maungu atamsamehe madhambi yake, hata kama
yatakuwa ni kiasi cha idadi ya nyota) [13].
3- KUTOA
SADAKA
Kiasi
kiwezekacho hata kama ni kipande cha tende.
Aliulizwa
Imam Swaadiq (a.s): Ewe mtoto wa Mtume wa Mwenyezi Mungu! ni tendo gani bora
kati ya matendo yafanywayo katika mwezi wa Shaaban? Akasema: (Ni kutoa sadaka
na kufanya istighfari, na mwenye kutoa sadaka katika mwezi wa Shaaban Mwenyezi
Mungu mtukufu atailea kama ambavyo mmoja wenu aleavyo mtoto wake hadi aweze
kulipwa siku ya kiama na imekua kubwa na kuwa kama mlima wa Uhud) [14].
4-KUSOMA
TAHLIIL (YAANI: LAA ILAHA ILLA LLAH)
Na
atafanya tahliil katika siku zote za mwezi mara elfu moja:
(لا
إله إلا الله ولا نعبد إلا إيّاه مخلصين له الدين ولو كره المشركون)
5-KUSALI
RAKAA MBILI
Kila
siku ya Al-khamisi ya mwezi mtukufu wa Shaaban.
Amesema
Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w): (Mwenye kusali rakaa mbili katika mwezi huu:
akisoma katika kila rakaa Suuratul-fatiha na Qul-huwallahu ahad) mara mia moja
na akitoa na kumsalimia Mtume (s.a.w.w) mara mia moja Mwenyezi mungu atamkidhia
haja zake zote kati ya mambo yake ya dini yake na dunia) [15].
6-KUSOMA
SWALAWAAT ILIYO POKELEWA KUTOKA KWA IMAMU WETU ZAINUL-ABIDIIN (A.S)
Kila
mchana kati ya siku za mwezi wa Shaaban na katika usiku wa nusu ya mwezi huo na
swalawat hiyo ni hii ifuatayo:
(بسم
الله الرحمن الرحيم، اللهم صلّ على محمد وآل محمد شجرة النبوة وموضع الرسالة
ومختلف الملائكة ومعدن العلم وأهل بيت الوحي و...).
7-KUSOMA
MUNAAJAATI ULIO POKELEWA KUTOKA KWA AMIRIL-MUUMINIIN (A.S)
Na ulio
maarufu kwa jina la (Al-munajaatish-shaabaniyyah na matni yake imo kwenye
vitabu vya dua.
[1]-Al-aamal cha Swaduuq.
[2] -Mustadraku wasaailu shia\
Juzu 7 \ Abwaabu swaumul-mandub \ Babu Istihbabul-istighfar wa…..fii shaaban\
ukurasa 544\ chapa ya Muassasah Aalul-baiti liihyaait-turaath\ chapa ya kwanza
1407 hijiria.
[3] -Al-amaal cha Swaduuq.
[4] -Tafsiri Majmaul-bayaan ya
Twabarasiy juzu\ 5.
[5]-Mustadraku wasaailu shia
juzu \ 7 chapa ya Muassasatu Aalul-baiti li’ihyaai turaath, Abwaabus-swaumu
al-manduub\ baabu istihbaabul-istighfari wa… fii shaaban \ukurasa 542.
[6] -Wasaailu shia \
kitaabus-swaumu \ Abuwaabus-swaumul-manduub \ Istihbaabu swaumu shaaban\
ukurasa 366 \ Daru ihyaau turaathil-arabiy \chapa ya nne 1219 hijira.
[7]-Chanzo kilicho tangulia.
[8]- Chanzo kilicho tangulia.
[9]-Chanzo hichohicho.
[10]-Chanzo kilicho tangulia.
[11]-Chanzo kilicho tangulia.
[12]-Tuhaful-ukuul \ baabu
kalimaatul-imam Ridhaa (a.s).
[13]-Mustadraku Safiinatul-buhaar
\ cha Namaaziy – juzu 5 \ 414.
[14]-Iqbalul-aamal cha Sayyid
ibnu Twaawus \juzu 3 \ 294.
[15]-Wasailu shia \ chapa ya
Aalul baiti \ juzu 8 \ 104.
Comments
Post a Comment