Licha ya ukweli
kwamba Arabia ilikuwa ni shimo la uovu na ngome ya ibada ya masamu na
ushirikina, Muhammad mwenyewe hakuwa kamwe amechafuliwa na inda au dhambi
yoyote, na kamwe hakuinama mbele ya sanamu lolote. Hata kabla hajatangaza
kwamba amekuja kusimamisha ufalme wa Mbinguni hapa duniani, tabia yake na
mwenendo wake mwenyewe vilikuwa ni kiakisi (picha) cha Qur'an Tukufu. Hata
wakosoaji wake hawakuweza kuonyesha tofauti kati ya tabia yake na maagizo ya
Qur'an wakati wowote, kabla na baada ya Tangazo.
Baada ya
Tangazo la ujumbe wake kama Mtume wa Mungu, aliziweka mila na desturi za
kipagani chini ya amri ya kupigwa marufuku, lakini hakuna ushahidi kwamba kabla
ya kufanya hivyo, yeye mwenyewe aliwahi kutenda jambo la kipagani, au hasa
tendo lolote lenye kukinzana na Qur'an.
Inaonekana
kwamba, Qur'an, kitabu cha Mungu kilikuwa kimegandamizwa kwenye moyo wa
Muhammad tokea mwanzo, na pia inaonyesha kwamba "alihubiri" Uislamu
hata kabla ya kubaathiwa, bali tu kupitia matendo yake na sio kwa maneno.
Matendo yake yalikuwa fasaha sawa kama ilivyokuwa hotuba zake, na yaliutangazia
ulimwengu ni vipi alivyokuwa mtu wa adabu. Hata hivyo walikuwa ni wale mapagani
waliomwita Amin (mwaminifu) na Sadiq (mkweli), na walikuwa ni
watu haohao ambao, katika miaka ya baadae, walimsumbua, wakamuwinda,
wakamfukuza, na kuweka na kutangaza malipo juu ya kupatikana kichwa chake.
Pamoja na
kupotoka na ukorofi, kama mapagani wa Kiarabu walivyokuwa, bado walivutiwa na
ukweli; hata ukiwa kwa adui. Bado kupendezewa kwao na ukweli wa Muhammad (s.a..w.w)
hakukuwazuia kutafuta kumuangamiza aliposhutumu ibada yao ya masanamu na
ushirikina wao. Walishikwa na kiu juu ya damu yake tangu pale alipowaita kwenye
Uislamu lakini hawakujiuliza kuhusu kuwa kwake mkweli. Juu ya hoja hii hapawezi
kuwepo na ushahidi wa kuaminika kabisa hasa zaidi ya wao.
Waislamu tunatakiwa tuwe na tabia
njema kama alivyokuwa Mtume wetu kiasi kwamba adui ashindwe kupata kisingizio
cha kutushambulia na kama akitushambulia kwa ujeuri dunia nzima itashuhudia
kuwa waislamu wanaonewa. Haikubaliki kwa muislamu kuwa mbabe na mwonezi ambayo
kazi zake ni kuwapiga na kuwadhalilisha wanadamu wengine.
Comments
Post a Comment