Mwezi wa Ramadhani unakaribia, waislamu tutaanza kushutumiana kuhusu mwandamo
wa mwezi. Kuna watu wanasema kuwa mwezi ukiandama popote duniani tufunge,
lakini cha kushangaza ni kuwa wao wanaangalia mwezi unaoandama Saudi Arabia tu
na wala sio nchi zingine. Najiuliza hizi ni siasa au dini? Mwaka jana kuna nchi
mbili za Afrika Magharibi, mwezi uliandama kabla ya Saudi Arabia lakini
hawakufunga, japokuwa taarifa ziliwafikia walizipinga na wakaendelea kuongoja
Saudi Arabia watangaze. Kama kweli ni utaratibu kufuata mwezi unaoandama popote
duniani, Saudi Arabia nao wafuate mwezi unaoandama huku kwetu. Kwa ukweli
watetezi wa hoja hii ni wale wanaopata mshahara kutoka serikali ya Saudi Arabia
na huu ni aina Fulani ya ukoloni.
Waislamu tuliowengi tunafuata hadith ifuatayo inayotuelekeza
kila eneo liangalie mwezi unaoandama katika eneo lao. Ibn 'Abbaas anamnukuu Kuraybu, "Ummul
Fadhli bint Harith [mama yake Ibn 'Abbaas] alinituma kwa Muawiyya katika mji wa
Shamu nikafika Shamu na kutekeleza haja zake [zote] na ukaonekana mwezisayari
wa mwezi wa Ramadhaan, na mimi nipo Shamu, tukauona mwezisayari usiku wa
kuamkiya Ijumaa, baada ya hapo nikarudi Madina mwisho wa mwezi [wa Ramadhaan]
akaniuliza Ibn 'Abbaas, kisha akautaja mwezi akasema: lini mliuona mwezi?
nikamwambia usiku wa kuamkiya Ijumaa. Akasema kuniuliza wewe umeuona usiku wa
kuamkiya Ijumaa? Nikajibu ndiyo na wameuona watu [wote] na wakafunga, na
akafunga Muawiyya [piya] akasema Ibn 'Abbaas lakini sisi tumeuona mwezi usiku
wa kuamkiya Jumamosi na tutaendeleya kufunga mpaka tukamilishe siku 30, au
tuuone[wenyewe], nikamwambiya [Ibn 'Abbaas] je, hukutosheka kwa kuuona Muawiyya
na kufunga kwake akajibu kwa kusema, "hivi ndivyo alivyotuamrisha Mtume
(Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)."
Sanad ya Hadith hii ni sahihi na haina shaka kwa mfano angalia
sanad ya Al-Tirmidhi utaona sanad inasema kwa uwazi: .."Katuhadithia
Muhammad bin Abi Harmala katupa habari Kurayb ". Na katika masimulizi ya
Abu Daud: ".Katupa habari Muhammad bin Abi Harmala katupa Habari
Kurayb". Na katika masimulizi ya Ibn Khuzaima: " Kutoka kwa Muhammad
(yaani bin Abi Harmala) kutoka kwa Kurayb". Na katika masimulizi ya
Al-Nasaai: " Katuhadithia Muhammad - naye ni Ibn Abi Harmala - kasema kanipa
habari Kurayb". Na katika masimulizi ya Al-Bayhaqi: "Kutoka kwa
Muhammad bin Abi Harmala kutoka kwa Kuraib".
KUMJADILI KURAYBU
KUMJADILI KURAYBU
Watukufu Waislam mpokezi
wa hadith hii Kurayb kama ilivyotajwa hapo juu. Labda tutahitaji kumjua kama ni
mwenye kuaminika. Kuraybu ni mtu ambaye wanachuwoni wa hadith wanamkubali kuwa
alikuwa mtu mkweli sana na anategemewa katika upokezi wa hadithi tazama kitabu
'Tahdhibu' cha Imam Ibn Hajar Al 'Asqalani [jalada la 3 uk 468 chapa ya Beirut
tazama mahala pa herufi kaaf] Na tazama vile katika Taqribu Tahdhibu cha huyu
huyu Ibn Hajar Al Asqalani jalada la 2, uk 28.
Comments
Post a Comment