MUDA SAHIHI KWA KUFUTURU
Allah (s.w) anasema katika Qur’an tukufu, “... na
kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu uzi mweupe katika uzi mweusi wa
alfajiri, kisha timizeni swaumu mpaka usiku. ... (2.187).
Kwa aya aya hii inabainika muda wa mwisho wa kula daku
na muda wa kufuturu. Kwa maana kwamba mwisho wa kula daku ni muda mfupi kabla
ya swalatil Sub-hi na mwanzo wa kufuturu ni usiku unapoingia. Tukiambiwa usiku,
sio msamiati usioeleweka, ninaamini kuwa kila mtu anajua hivi sasa ni usiku au
la.
Lakini kwa bahati mbaya baadhi ya ndugu zetu katika
imani wamekuwa wakifuturu mchana kweupe badala ya usiku. Wao huhimizana kuwa “cheleweni
kula daku na harakisheni kufuturu” na kuyanasibisha maneno haya na kauli ya
Mtume (s.a.w.w). Maneno haya hayawezi kukubaliwa kiurahisi bila kuyafanyia
uchambuzi ili tujue utekelezaji wake ukoje.
Je, kama aya inatuagiza tufunge mpaka usiku, Mtume (s.a.w.w)
anaweza kuagiza kinyume chake? La hasha Mtume hakuwahi kwenda kinyume cha Qur’an
hata siku moja. Hivyo aidha hiyo hadith itakuwa ni ya uongo au watumiaji wa
hadith hiyo wameipotosha maana.
Hivi kama hadith inasema wahini kufuturu, imetuwekea
muda? Hapana, hadith hiyo haina muda wa kufuturu. Kwa maana hii bila shaka
imepotoshwa maana na masheikh kwa maslahi yao binafsi. Kuwahi kufuturu ina
maanisha kuwa pindi usiku unapoingia tuwahi kufuturu na sio kuwafuturisha watu
bado mchana peupe kwa madai ya kuwahi kufuturu.
Utasikitishwa na baadhi ya misikiti ambapo huwahi
kuadhini, bado peupe kiasi kwamba ukiwaambia watu muda huu ni usiku watapinga
na wala hakuna mtu hata mmoja anayeweza kukubali huwa muda huu ni usiku. Wakati
huo baadhi ya watu hugawa tende na kuwahimiza watu wazile haraka haraka kabla
ya hata ya swala ili wao wapate thawabu za kuwafuturisha. Lakini kwa bahati
mbaya watu hawa watapata dhambi ya kuwafunguza swaumu watu waliowapa tende
badala la kupata thawabu kwa sababu muda wa kufuturu unakuwa bado.
Comments
Post a Comment