NISABU YA NG'OMBE (KIWANGO
CHA KUTOLEA ZAKA)
Ng'ombe wakiwa chini ya 30
hawatolewi Zaka.
Kutoka 30 mpaka 39 atatolewa
ndama mmoja wa umri wa mwaka mmoja. kutoka 40 mpaka 59 atatolewa ndama mmoja wa
umri wa miaka miwili. Kutoka 60 mpaka 69 watatolewa ndama wawili wa umri wa
mwaka mmoja mmoja. Kutoka 70 mpaka 89 atatolewa ndama mmoja wa umri wa mwaka
mmoja na ndama mmoja
wa umri wa miaka miwili.
Kutoka 90 mpaka 99 watatolewa
ndama 3 wa umri wa mwaka mmoja mmoja. Kwa ng'ombe 100 watatolewa ndama 2 wenye
umri wa mwaka mmoja na ndama mmoja mwenye umri miaka 2. Wakizidi hapo ndama
mmoja wa umri wa mwaka mmoja atatolewa kwa ng'ombe 30 na ndama mmoja wa umri wa
miaka miwili kwa ng'ombe 40. Ng'ombe wanaofanya kazi shambani hawahesabiwi
pamoja na wale wanaotozwa Zaka.
Comments
Post a Comment