TAREHE YA KUZALIWA MTUME (s.a.w.w)
Katika kitabu cha historia cha Qadhi
Husain Ibn Muhammad Diyar
Bakari al-Maliki inayoitwa Tareekh-e-Khamees, imeandikwa hivi kwamba
Mtume wetu alizaliwa mwezi kumi (10) Rabi-ul-Awwal,
na kwa mujibu wa walivyopokea wengine,
tarehe ya kuzaliwa kwake ni kumi na mbili (12) Rabi-ul-Awwal na wengine
wamepokea kuwa ilikuwa kumi na saba (17) Rabi-ul-Awwal. Kwa nchi za kiislamu
kama Iran wiki nzima ya kuanzia 12 mpaka 17 huwa ni wiki ya sherehe ya kuzaliwa
Mtume (s.a.w.w) ili waislamu wa madhehebu yote washiriki katika ibada hii
muhimu ya kukumbuka kuzaliwa kwa kiongozi wa Ummah huu. Wiki hii huitwa wiki ya
umoja na watu hawaende kazini kwa wiki nzima.
Suala la mwaka halina ubishi kwani wote
wameandika kuwa kwa kalenda ya waarabu kipindi hicho, mwaka aliozaliwa Mtume (s.a.w.w)
ulikuwa ukiitwa mwaka wa tembo (A’mul fiil). Isipokuwa waandishi
wamekhitilafiana tena kuwa mwaka huo unalingana na mwaka gani ya miladia au
Gregorian callender. Wapo waliosema ni mwaka wa 570 AD na wengine walisema kuwa
ni mwaka 571 AD.
Comments
Post a Comment