TAUHID KATIKA USAHIHI WAKE.

Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Je, kuna muumba asiyekuwa Mwenyezi Mungu"  Qur'an, 35:3
Na Amesema tena:
"Waambie, Mwenyezi Mungu ndiye muumba wa kila kitu" Qur'an, 13:16.
Umma umekubaliana juu ya Tauhidi yake katika Rububiya yake na kwamba hapana Mola wala mwenye kusimamia (mambo yao) asiyekuwa yeye.
Amesema Mwenyezi Mungu:
Yeye ndiye anayesimamia mambo yote hakuna muombezi ila baada ya idhini yake, huyo ndiye Mwenyezi Mungu Mola wenu basi muabuduni yeye, Je, hamna kumbukumbu?
Pia wamekubaliana kumpwekesha Mwenyezi Mungu katika Ibada na kwamba, yeye Mwenyezi Mungu ndiye Mola ambaye anastahiki kuabudiwa na hakuna wa kuabudiwa asiyekuwa Yeye.
Mwenyezi Mungu Amesema:
"Waambie, Enyi mliopewa Kitabu, njooni kwenye neno lililo sawa kati yetu na ninyi ya kwamba, tusimuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu, na wala tusimshirikishe na chochote, wala baadhi yeta tusiwafanye kuwa waungu badala ya Mwenyezi Mungu". Qur 'an, 3:64
Bali hizi ndizo nukta ambazo zenye kuafikiana baina ya sheria za mbinguni. Basi mtazamo ulio kinyume na misingi hii ni miongoni mwa vitendo vya uchafuzi na kupotoshaji.

Na wapotoshaji hao si wengine bali Mawahhabi ambao wanajifanya kuwa wanajifanya kuwa wanafuata tawhiid halafu wanapotosha dhati ya Mwenyezi Mungu ili waweze kuwakufurisha waislamu wa kisawasawa ambao ni Mashia na ndugu zao AhlulSunnah waljamaa. 

Comments