Imani hii potofu inatokana na fikia
ya Sheikh mpotofu aitwaye Ibn Taimiyyah ambaye ametuarifisha maana ya Tauhidi
katika kitabu chake aliposema: "Hakika Mwenyezi Mungu yuko juu ya mbingu
yake kwenye arshi yake, yuko juu ya viumbe wake"
Na amesema
tena: "Mola wetu hushuka mpaka kwenye mbingu ya dunia kila siku inapobakia
theluthi ya mwisho ya usiku kisha husema; Nani ataniomba (saa hizi) nami
nitamkubalia (maombi yake), nani ataniomba nami nitampa, ni nani atanitaka
msamaha nami nitamsamehe".
Haya ndiyo
maarifa ya sheikh huyu ambayo wao humwita sheikhul Islam (Ibn Taimiyyah) na
huku ndiko kumtakasa kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu na (yote haya aliyoyasema)
inajulisha wazi kabisa kuwa yeye anaitakidi kuwa Mwenyezi Mungu anao mwili na
anapatikana upande fulani. Na (huyu Ibn Taimiyyah) amesema hayo kutokana na
kung'ang'ania kwake dhahiri ya aya na hadithi za Mtume bila ya kuzitafiti kwa
undani aya zilizokuja kuhusu maudhui hiyo, na bila ya kufanya uhakiki katika
isnadi za hadithi na madhumuni yake.
Imani hii
potofu ilirithiwa na masheikh wengine wa kisalafiya na Answar Sunnah kama Ibn
Al-Qayyim na Muhammad bin Abdul-Wahhab. Na cha ajabu ni kwamba, hawa nao
wanataka wawe ni waalimu wa Tauhidi na walinganiaji wa Tauhid.
Rejea:
Maj-mu'a 'Tur-Rasailil-Kubra, cha Ibn Taimiyyah,
Al-A'qidatul-Wasitiyah uk. 401.
Watu hawa kwa
sababu ya kung’ang’ania kutafsiri aya za Qur’an na hadith za Mtume bila ya
kusoma Uislamu kwa undani wake wamekuwa wakichagua aya zinazohimiza vita na
kuzitafsiri vibaya kama ushahidi wa kuwauwa na kuwadhalilisha wanadamu, na
kuzitupilia mbali aya nyingi tu za Qur’an ambazo zinahimiza upendo, amani na
umoja. Vile vile Qur’an tukufu inahimiza watu wawe wasamehevu lakini wao
wanafundisha wafuasi wao wawe wababe na wajeuri.
Comments
Post a Comment