Shukurani zote zinamsitahiki Mwenyezi
Mungu,na rehma na amani zimuendee Mtume wetu Muhammad, na ahli zake na
maswahaba zake waliokuwa wema.
Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Sema; Enyi
watu mlio pewa kitabu (cha Mwenyezi Mungu. Mayahudi na Wakristo)! njooni katika
neno lililo sawa baina yetu na baina yenu; ya kwamba tusimuabudu yeyote ila
Mwenyezi Mungu,wala tusimshirikishe (Mwenyezi Mungu) na chochote,wala baadhi
yetu tusiwafanye wengine kuwa waungu badala ya Mwenyezi Mungu (au pamoja na
Mwenyezi Mungu). wakikengeuka, semeni: Shuhudieni ya kwamba sisi ni waislamu, (tumenyenyekea
amri za Mwenyezi Mungu”).1
1 Al imran: 64
2 Al aaraf :33
Kwa hakika dini ya Uislamu ndiyo dini ya
haki, kwa kuwa ndio dini ya kimaumbile iliyo sahihi, dini iliyo wazi ambayo
hakuna ndani yake ugumu wowote wala uficho wa aina yeyote, kila mtu katika Uislamu
ana haki ya kuuliza chochote kinacho mtatiza, au jambo lolote linalo msumbua
katika akili yake.
Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: “ Sema
(uwaambie): “Mola wangu ameharamisha mambo machafu, yaliyodhihirika na yaliyo
fichika, na dhambi na kutoka katika utii (wa wakubwa) pasipo haki, na
kumshirikisha Mwenyezi Mungu katika ambacho hakukiteremshia dalili (ya kusema
kishirikishwe naye) na (ameharamisha)kusema juu ya Mwenyezi mungu msiyo yajua”.2
Bali Uislamu umetoa haki ya kujibu mambo
yanayo fungamana na dini kwa watu wenye elimu ya kisheria, amesema Mwenyezi
Mungu mtukufu: “… Basi waulizeni wenye kumbukumbu (za vitabu vya Mwenyezi Mungu
vya kale) ikiwa nyinyi hamjui’3
3 Annahli :43
Anayeulizwa ni bora awe mjuzi kweli kweli
kwa sababu kama ukipata maarifa kwa mtu asiye na ujuzi sahihi wa Uislamu basi
atakupotosha na utajikuta unakuwa mwislamu wa ajabu ajabu kama vile takfir.
Tunamwomba Allah atuepushe kuwafuata watu
wajinga na pia atuepushe kuwa katika makundi ya watu wanaofuata maslahi ya
kidunia na kuisahau akhera huku wakiitaka.
Comments
Post a Comment