ULAWITI NI DHAMBI KUU

Kwa upande wa Madhehebu ya Shia Ithnaashara: Mojawapo ya madhambi ambayo yamechambuliwa kama ni miongoni mwa dhambi kuu ni ulawiti au kuingiliana jinsia moja. Hivyo imethibitishwa na al-Imam as- Sadiq (a.s.) na Al-Imam Ali ar-Ridha (a.s.). Kwa hakika dhambi hili ni kubwa hata kuzidi dhambi ya zinaa. Madhambi na adhabu yake ni zaidi ya zinaa. Amesema al-Imam as- Sadiq (a.s.) katika Al-Kafi :
“Kuingiza uchi wako mwanzoni mwa sehemu ya nyuma ni dhambi kubwa kabisa hata kuliko kuingizia katika uke. Kwa hakika Allah (swt) ameangamiza ummah mzima wa Mtume Lut (a.s.) kwa sababu wao walijiingiza katika laana ya ulawiti. Allah (swt) kamwe hakumteketeza hata mtu mmoja kwa dhambi ya zinaa.”

Amesema Mtume Muhammad (s.a.w.w.) katika Wasa’il al-Shiah :

“Mtu yeyote anayetenda ulawiti pamoja na kijana wa kiume atapatwa na janabah (uchafu) ambao hautaweza kutakasishwa hata kwa maji ya dunia nzima. Allah (swt) atamghadhabikia na kumlaani vikali. (Yaani Allah swt atazichukua rehema na baraka kutoka kwake na kumlipa Moto yaani Jahannam). Kwa hakika ni mahala pabaya kabisa! Pepo (Jannah) zitakuwa zimemkasirikia mno. Na mtu ambaye anakubali kulawitiwa kwa nyuma, basi Allah (swt) humweka ukingoni mwa Jahannam (motoni penye moto mkali kabisa) na atamweka huko hadi hapo atakapo maliza kuwahoji watu wote. Hapo ndipo atakapo mwamrisha kuwekwa Motoni rasmi. Atapitia adhabu moja baada ya yapili hadi kuzimaliza adhabu zote za Jahannam na hadi atakapofikia daraja la chini kabisa. Na kamwe hataweza kutoka hapo.”

Comments