UMAR
BIN KHATAB, KHALIFA WA PILI KUPITIA WAPINZANI WA MTUME (S.A.W.W)
Kipindi kabla ya Uislamu Umar alikuwa dalili na kabla
ya hapo alikuwa mchungaji wa ngamia. Kipindi hiki Umar alikuwa adui mkubwa wa
Mtume na waislamu kwa ujumla. Yeye aliukubali Uislamu baada ya miaka sita tokea
Mtume (s.a.w.w) atangaze utume wake.
Baadhi ya wanahistoria wanadai kuwa Umar bin Khatab
alikuwa shujaa kiasi kwamba kuingia kwake katika Uislamu kuliwatia hofu kweli
kweli waabudu masanamu. Lakini ukweli unaonesha kinyume cha hayo. Kwani wakati
Umar alipoukubali Uislamu makafiri walibaki na ukafiri wao na hakuna chochote
kilichobadilika. Badala ya kupata ahueni tulishuhudia Mtume wetu akilazimika
kuikimbia nyumba yake kwa miaka mitatu akaishi katika pango kwa amri ya
Maquraish, kipindi hiki alikumbana na njaa kali sana na mazingira
yanayohatarisha maisha yake. Kipindi hiki Umar na Abubakar walikuwa Makah
wakila kuku kwa mrija na hawakuchukua hatua yoyote iwe ni kuzuia tatizo hili au
kumsaidia Mtume na familia yake waliokuwa wanateseka kwa njaa.
Miaka michache baadaye Mtume alilazimika kuikimbia
Makah na kwenda kwanza Taif ambako alikumbana na madhila makubwa kuliko hata ya
Makah na kisha baadaye alihamia kwenda Madina. Kabla ya kuondoka Maka makafiri
walikuwa wameizunguka nyumba ya Mtume tayari kwa kumuua. Je Umar na ushujaa
wake alifanya nini ili kumnusuru Mtume katika hali hii ngumu?
Baada ya Mtume (s.a.w.w) kufika Madina na Masahaba
kumfuata, alitengeneza undugu baina ya masahaba ili waweze kusaidia kutokana na
kwamba Muhajirina walikuwa wameacha familia zao Makah hivyo wanahitaji familia.
Katika tukio hili Mtume alimpanga Imam Ally kuwa ndugu yake na Umar akapangwa
kuwa ndugu wa Utban bin Malik.
Katika mwaka wa tatu bint wa Umar aitwaye Hafsa
aliolewa na Mtume
Umar
bin Khatab alikimbia Jihad mara kadhaa. Mojawapo ni vita Uhudi kiasi kwamba
Yeye mwenye Umar anasema kuwa nilikimbilia mlimani (Suyuti katika Al-Durrul
Al-Manthur). Katika vita vya Khaibar Umar aliongoza jeshi lakini akashindwa
kuleta ushindi. Katika vita vya Hunain alikimbia vita kiasi kwamba Abu Qatada
mmoja wa Masahaba wa Mtume anasema kuwa katika vita ya Hunain wakati waislamu
walipokimbia vita, nami nilikimbia na nikamwona Umar na wengine wengi
wakikimbia (Bukharin a Kitabul Maghazi).
Katika
mwaka wa nane Hijriya Umar alitumwa na Mtume katika vita iitwayo Dhat es
Salasil, chini ya uongozi wa Amr bin Aas kama kamanda.
Mwaka
wa 11 Hijriya, Mtume aliandaa jeshi kwenda Syria na akamteua Usama bin Zaid bin
Hatith kama kamanda. Mtume alimwamuru Umar ajiunge na jeshi la Usama.
Pamoja
na kwamba Umar aliishi na Mtume kwa miaka 18 akiwa sahaba wake, hakuweza kupewa
cheo chochote na Mtume kiwe cha kiraia au kijeshi isipokuwa kimoja tu kile cha
kuongoza vita vya Khaibar ambapo alishindwa vibaya sana na kukimbia. Ushindi
ulipatikana kesho yaka chini ya uongozi wa Imam Ally (a.s).
Tutaendelea
na Historia hii ya Khalifa Umar bin Khatab Inshallah.
Comments
Post a Comment