UMUHIMU WA SWALA

UMUHIMU WA SWALA
 “ewe Mola wangu Mlezi! nijaalie niwe msimamishaji Swala na kizazi changu, Mola wetu! na upokee maombi yangu”1
Anasema Imam Al- Baqir (a.s): “Kitu cha kwanza atakachohesabiwa muumini (Siku ya Kiyama) ni Swala, ikikubaliwa yatakubaliwa matendo mengine, na ikikataliwa basi yatakataliwa matendo mengine.”2
Nadhani unafahamu kuwa kama matendo yako yote yakikataliwa na Allah (s.w.) itakuwa na maana kuwa wewe ni mtu wa jahanamu.
Rejea:
1. Sura Ibrahim: 40.
2. Biharul-An'war, Juz. 47 Uk. 2.

Hivyo basi hakuna mjadala, endapo kama unataka kuokoka kutokana na adhabu ya Allah (s.w) huna budi uanze kuswali leo. Usingoje maana hujui utakufa lini? Kwa bahati nzuri huu ni mwezi wa Ramadhani ambao ni mwezi wa toba, akianza ibada ndani ya mwezi huu na ukatubia na kuazimia kuwa hutorejea kufanya maovu tena,basi Allah (s.w) atakusamehe, insha-Allah. 

Comments