USHAHIDI WA IMAM ALLY (A.S) KUDHULUMIWA UKHALIFA

USHAHIDI WA IMAM ALLY (A.S) KUDHULUMIWA UKHALIFA
Kuna watu wananihoji kama ninaushahidi wa kuthibitisha kuwa Imam Ally (a.s) alidhulumiwa ukhalifa na Abubakar bin Quhafa. Nimetafuta katika vitabu na hatimaye nimeupa ushahidi mzuri sana. Kwa sababu msemaji ni yeye Mwenye Abubakar na pili kitabu nilichokirejea ni cha Kisunni. Baada ya hili ninawaombeni wote sasa mmuunge mkono Imam Ally (a.s) na Ahlulbayt wa Mtume (s.a.w.w) kwa ujumla.
Ibn Abil Hadid Mu'tazil katika Sharh-e-Nahajul Balagha jz 4 uk 80 ameandika kuwa Abubakar swidiq alimtukana Ally bin Abu Twalib na bibi Fatwima (a.s) kama ifuatavyo "enyi watu! Kwa nini mnachanganyikiwa hivi? Kwa nini mumsikilize kila mtu? Kwa vile tu nimekataa ushahidi wao wanazungumza upumbavu. Ukweli ni kwamba yeye ni mbweha ambaye amesalitiwa na mkia wake... Yeye ni sawa na ummu't-tihala ambaye watu wa nyumbani kwake mwenyewe walipendelea kuzini naye"

Haya ndio maneno ya Abubakar akithibitisha kuwa Imam Ally amesalitiwa na watu wake na pia akidai kuwa kulalamika kwake ni upumbavu mtupu kwa sababu hata afanyeje hawato mrejeshea ukhalifa bali wataendelea kuwatesa Ahlulbayt mpaka wakubali kuwa chini ya utawala wao wa haramu.

Comments