VITABU VYA KIISLAMU JINSI VILIVYOCHAKACHULIWA KUFICHA UKWELI.

 at-Tarikhat-Tabari, chapa ya Leiden (ya mwaka 1879 Miladia) kimeyanakili maneno ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w) aliyoyatumia wakati wa karamu mashuhuri ya ndugu wa karibu aliyoitayarisha ambapo katika khutba yake alisema: “Enyi watu wangu! Huyu Ali ni ndugu yangu, Wasii wangu na Khalifa wangu miongoni mwenu; msikilizeni na mtiini.” Lakini katika chapa ya Misri ya mwaka 1963, (chapa inayodaiwa kuwa imechekiwa na ile ya Leiden) maneno haya muhimu: “Wasii wangu na Khalifa wangu” yamebadilishwa na kuandikwa “kadha wa kadha” na kusomeka hivi: “Huyu Ali ni ndugu yangu na kadha wa kadha.”
Huu ni msiba mkubwa. Huu ni mchezo umefanywa na unaendelea kufanywa mpaka leo. Na lengo ni kuficha ukweli. Lakini hata hivyo, ‘ukweli siku zote unaelea’; matoleo ya zamani yapo mengi na yamehifadhiwa kwenye maktaba zetu.

Ni muhimu kufikia kila aina ya maoni katika kujaribu kuamua ukweli.
Uislamu kimsingi uko dhidi ya kufuata kibubusa. Utafiti huu umefanywa ili kuwaelemisha Waislamu kwa ujumla juu ya madhehebu za Kiislamu ili kujenga maoni yao kuhusu mtazamo mzuri wa mtu mwenyewe, na ni muhimu mtu kuelewa hoja za wale ambao hakubaliani nao. Inawezekana kusemwa kwamba wale ambao hawaelewi kabisa mtazamo wa maoni tofauti, hawaelewi kwa ukamilifu (mtazamo) wa kwao wenyewe.

Hivyo tuendelee kufanya utafiti na tumwombe Allah atuonyesha haki kuwa hii ni haki aturuzuku kuifuata na pia atuonyeshe bayana kuwa hii ni batili na atuepushe kuiacha. Jibu ameen. 

Comments