WITO WA MTUME MUHAMMAD (S.A.W.W).

Mtume (s.a.w) ali walingania  watu  kwenye   upweke wa Mwenyezi Mungu katika mji wa makka na kwa njia ya siri kwa muda wa miaka mitatu, na baada ya kipindi cha siri ali waita watu kwa njia ya wazi kwa muda wa miaka kumi.
KUHAMA KWAKE.
Alihama kutoka katika mji wa makka kwenda madina  mwanzoni mwa mwezi wa rabiul awwal baada ya kupita miaka  13 tangu kupewa utume, na kuhama huko kulitokana na maudhi mengi ya makuraishi, mushrikina na mkafiri  kumuelekea yeye na maswahaba wake. Kiasi kwamba maswahabi wengi waliuawa na makafiri wa kikuraishi kiasi kwamba alilazimika kuwatorosha waislamu na kuwapeleka Ethiopia ili wapishe mateso na dhuluma wanazofanyiwa na makafiri wa Maka. Walioteswa sio Masahaba pekee bali hata yeye mwenyewe na familia yake.
Ukoo wa Mtume (s.a.w.w) uliwahi kuwekewa vikwazo kwa muda wa miaka mitatu kiasi kwamba walifukuza mjini Maka na  kwenda kuisha katika pango la Abutalib kiasi kwamba hawakuruhusiwa kuuza kitu wala kununua na wala hawakuruhusiwa kuingia mjini. Utakumbuka vilevile kuwa siku moja alifunga safari kwenda katika mji wa jirani iitwao Taif na huku alikuta watu wamejipanga mistari na kumshambulia kwa kila silaha na kulazimu kurudi Maka bila kufanya tabligh katika mji huo.
Wale wanaosema kuwa Uislamu unaenezwa kwa nguvu wamekosea sana. Uislamu unaenezwa kwa mahubiri tu. Kama ingekuwa utumiaji nguvu kuutangaza Uislamu linaruhusiwa katika Uislamu basi tungeshuhudia Mtume akipambana na watu kuwalazimisha waingie katika Uislamu. Kama watu walilazimishwa kuukubali Uislamu basi hilo lilifanywa na madikteta walionyakua utawala wa dini ya Kiislamu na kuugeuza kuwa ni ufalme. Na Qur’an inatuambia bayana kuwa wafalme wakiingia katika miji huiharibu miji hiyo na kuwadhalilisha wakazi wa miji hiyo. Hiyo ndio kazi iliyofanywa na watu waliopora madaraka ndani ya Uislamu na kuwachinja wengi sio tu wa wasiokuwa waislamu bali waliwachinja waislamu wengi zaidi kuliko wasiokuwa waislamu.

Kazi hii ya ufedhuli inaendelezwa na maadui wa Allah waitwao Mawahhabi ambao wameshamirisha vita zao za kiibirisi na kuwachinja na kuwalipua watu katika dunia nzima. 

Comments