ZAKAT

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwingi wa ukarimu.
ZAKAAT kwa Kiarabu ni neno lenye maana mbili: (1) kuongezeka, na (2) kutakasika. Katika
sheria ya Kiislamu maana yake ni kutoa sadaka sehemu maalumu ya Mali liyoichuma Mwislamu kwa njia ya halali.

Kutoa Zaka ni nguzo ya katika nguzo tano za Kiislamu kwa upande wa Sunni na pia ni tawi katika matawi ya dini kwa mujibu wa Madhehebu sahihi zaidi katika Uislamu, nayo si nyingine bali Shia imamiya; na kila Mwislamu, mwanamume
au mwanamke, akiwa na kipimo maalumu cha mali, amelazimishwa kuitoa. Zaka imetajwa
pamoja na Sala ndani ya Kurani Tukufu na hilo laonyesha jinsi ilivyo muhimu amri hii.

Mwenyezi Mungu alimwamrisha Mtume Muhammad s.a.w. kuchukua sadaka kwa Waislamu.
Akasema “Chukua sadaka katika mali zao, uwasafishe kwayo na kuwatakasa, na uwaombee. Hakika kuomba kwako ni utulivu kwao; na Mwenyezi Mungu ndiye Asikiaye, Ajuaye.” (9:103).
Baada ya kufariki Mtume s.a.w. Makhalifa wake waliendelea kupokea sadaka hiyo kwa
Waislamu, na wakati mmoja baadhi ya Waislamu walipokataa kutoa Zaka, Seyidna Abu Bakr, Khalifa wa kwanza wa Mtume kwa mujibu wa Masunni, Mungu awe radhi naye, akawa tayari kupigana nao, akatangaza
kwamha hataacha kuwapiga vita watu hao mpaka watoe kile kipande cha kamba cha kufungia goti la ngamia walichokuwa wakitoa zama za Mtume s.a.w. Maana yake, Mwislamu ambaye anayo mali wala hatoi sehemu yake iliyolazimishwa na Mwenyezi Mungu hawi Mwislamu tena
Tena amesema Mwenyezi Mungu, "Na kama wakitubu na kusimamisha Sala na kutoa Zaka, basi ni ndugu zenu katika dini" (9:11). Bila shaka kutoa Zaka kunaimarisha udugu wa Uislamu, na mwenye kuitoa tu ndiye ndugu ya Waislamu wengine.


Kutokana na hili Khalifa wa Kiwahhabi Abubakar bin Quhafa (R.A) ALIWAUWA MASAHABA WENGI KWA KUGOMA KULIPA ZAKA KWA SABABU YA KUTOUTAMBUA UONGOZI WAKE ULIOPATIKANA KIUTATA NA UBABE KWA KUWATISHA WATU KUWAUA NA HAKIKA WALIWAUA BAADHI YAO. Mmoja wa walioua ni Maliki ambapo kamanda wa majeshi ya Abubakar kwa kipindi hicho akiitwa Khalid bin walidi alimbaka mjana wa Maliki jirani tu na maiti ya mme wa mama huyo. Huu ni msiba mwingine ulioukumba uislamu kwa watawala kulazimisha twa’ toka kwa waumini, hata pale ambapo hawakuistahili kwani tayari Mtume (s.a.w.w) aliache amemtangaza Imam Ally kuwa khalifa wake wa kwanza. 

Comments