BAHLUL AJIBU SWALI KUTOKA KWA KHALIFA HARUN.

BAHLUL AJIBU SWALI KUTOKA KHALIFA HARUN.
Siku moja khalifa wa Mawahabi yaani, Harun Rashid alikuwa katika Qasri yake akiangalia mandhari iliyokuwa ikimzunguka na sauti ya mbubujiko wa maji ya mto Tigris.

Na mara hapo akatokezea Bahlul, na Harun alimwambia Bahlul: "Ewe Bahlul! leo hii nakuuliza fumbo, iwapo utafumbua vyema basi nitakupa dinar elfu moja na iwapo utashindwa basi nitatoa amri ya kukutosa majini." Bahlul alimwambia Harun: "Mimi sihitaji dinar hizo, bali ninakubali kwa sharti moja." Na alipokubali Harun, Bahlul alisema: "Iwapo nitaweza kulijibu vyema basi itakubidi kuwaachia (Mashia) marafiki zangu mia moja - kutoka Gereza lako, na iwapo nitashindwa basi unao uhuru wa kunitupa majini."

Alianza Harun kulielezea fumbo lake: "Iwapo mimi ninaye mbuzi mmoja, mbwamwitu, na fungu la majani.Je nitawezaje kuvivusha vyote hivyo, kwamba majani hayataliwa na mbuzi na wala mbuzi kuvamiwa na mbwamwitu?"

Bahlul alianza kumjibu: "Kwanza utamvusha mbuzi kwenda ng'ambo ukimwacha mbwa mwitu na majani. Baadaye utachukuwa majani uyavushe huku ukirudi na mbuzi upande huu. Utamwacha mbuzi upande huu na utamchukua mbwamwitu ng'ambo. Mwishoni utampeleka mbuzi. Kwa hivi majani hayataliwa na mbuzi wala mbuzi kuvamiwa na mbwamwitu."
Harun alifurahishwa mno kwa majibu ya Bahlul. Na hapo Bahlul alimpa orodha ya majina mia moja ya wafuasi na wapenzi wa Ali bin Abi Talib (a.s. ).

Lakini Harun alimgeuka Bahlul na akagoma kuwaachia huru Mashia waliokuwa wamejaa magereza. Kwa upande wake, Bahlul aliendelea kusisitiza, na hatimaye aliwaacha huru watu kumi tu na akimwamwuru Bahlul kuondoka.

FUNDISHO.
1.  Baada ya Mtume (s.a.w.w) kufariki wafuasi wake na wafuasi wa khalifa aliyemteua kuongoza baada yake yaani imam Ally (a.s) waliteswa, kufungwa na kuawa na watawala waliodai kuwa wao ndio makhalifa hasa. Hii ndio sababu ya Mashia kuwa wachache kwani mpaka leo wafuasi wa makhalifa hao waovu hawaridhiki mpaka wao ndio wawe watawala, na wanapotawala kazi zao ni kuwauwa waislamu wasio na hatia maadamu wanatofautiana nao kimtazamo.
2.  Makhalifa hao walikuwa ni wanafiki kwa sababu ukichukulia mfano wa Harun Rashid katika tukio hili alitoa ahadi, na Allah katika Qur’an anatuambia ahadi lazima itimizwe na siku ya kiama utaulizwa lakini hakujali na akamdanya Bahlul kama ulivyosoma mwenyewe.

3.  Waislamu tuendelee kuusoma Uislamu kwa undani ili tuwe pamoja na wakweli na kujiepusha na kundi la waovu waliowafunga na kunyonga mashia na waislamu wengine waliotofautiana nao kimtazamo. Kumbuka suala la kutofautiana wanadamu ni la kimaumbile na hakuna sababu ya kuuana. 

Comments