BAHLUL AUZA PEPO
Siku moja Bahlul alikuwa ukingoni mwa mto
akicheza kwa udongo kwa kutengeneza nyumba na bustani.
Hapo alitokea Zubeidah, mke wake Harun
Rashid (khalifa wa Mawahhabi na Masalafi), akipita hapo. Alipomkaribia Bahlul,
alimwuliza: "Ewe Bahlul! Je wafanya nini?" Bahlul alimjibu:
"Najenga Pepo (Jannat)."
Zubeidah alimwambia: "Je wauza hizi
Pepo ulizozijenga?" Bahlul alimjibu: "Naam ninaziuza!" Zubeidah
alimwuliza: "Je kwa Dinar ngapi?" Bahlul alimjibu "Kwa Dinar mia
moja tu!"
Kwa kuwa Zubeidah alikuwa akitaka kumsaidia
Bahlul, hivyo aliona hapo ndipo pahala pa kumsaidia na alimwamuru mfanyakazi
wake amlipe Bahlul hizo fedha. Nao walimlipa hizo
dinar mia moja.
Usiku ule Zubeidah aliota ndoto akiwa
Peponi ambamo kuna Qasri nzuri mno iliyopambwa mno na wapo wajakazi wamesubiri
amri, wao walimwambia hiyo ndiyo Qasri aliyoinunua kutoka kwa Bahlul. Zubeidah
alipoamka siku ya pili, akiwa amejawa na furaha, alimwelezea mume wake,
Harun. Harun alimwita Bahlul, alipofika,
Harun alimwambia, "Ewe Bahlul, chukua hizi Dinar mia moja na uniuzie Pepo
mojawapo ya Pepo kama ile uliyomwuzia Zubeidah."
Bahlul alicheka na kumwambia: "Zubeidah
alinunua bila ya kuona ambapo wewe unataka kununua baada ya kujua ya kuwapo kwake. Hivyo
sitakuuzia!"
MAZINGATIO.
1.Mtu mwovu anaweza kuwa na mke au mme
mcha Mungu. Hivyo asihukumiwe mtu kwa sababu ya mkosa ya ndugu yake au rafiki
yake. Harun Rashid pamoja na kuwa alikuwa mwovu aliyepindukia hasa kwa kuwaua
waislamu wafuasi wa Mtume na Ahlulbayt wake (Mashia) lakini alikuwa na mke
mwislamu sahihi aliyekuwa na huruma na wanadamu wote ikiwemo Mashia.
2. Imani
ya kidini imejengwa juu ya kuamini mambo yasiyoonekana. Hivyo ukijifanya wewe
ni myakinifu, unataka uone kitu ndipo ukiamini basi dini itakushinda.
Tunatakiwa tusikiapo jambo la dini tuhoji kusihi kwake na tukiridhika tufuate
mara moja hata kama halionekani.itakuta baadhi ya watu tukiwaambia Allah
haonekani wanakuwa wakali na kudai kuwa ni lazima aonekane. Hawa wanafanana na
Harun Rashid
Comments
Post a Comment