ITIKADI YA SHIA ITHNA
ASHARIA KUHUSU DHATI YA ALLAH (S.W) IMETAKASIKANA ISIYOKUWA NA MWISHO.
Sisi tunaamini kuwa
dhati ya Mwenyeezi Mungu imeenea sehemu zote, naye hana mwanzo wala
mwisho, dhati hiyo inaonekana katika elimu yake, qudra ya utukufu wake, kubakia
kwake milele katika sehemu zote na zama zote, na kwa sababu hiyo basi ndio
tukasema kuwa Mwenyeezi Mungu hana sehemu maalumu wala kipindi maalumu, kwa
sababu sehemu au nafasi na zama zina kiwango maalumu, japokuwa Mwenyeezi Mungu
hana sehemu maalumu wala zama maalumu lakini Yeye yuko katika sehemu na zama
zote, kwa sababu dhati ya utukufu wake ni iko juu zaidi kuliko sehemu na zama,
kama tunavyosoma ndani ya Qur-an:-
Na Yeye ndiye Mungu
mbinguni, na ndiye Mungu katika ardhi. Naye ndiye Mwenye hikima, Mwenye ujuzi 5.
Yeye ndiye aliye ziumba
mbingu na ardhi katika nyakati sita; kisha akakaa vyema juu ya enzi. Anayajua
yanayo ingia katika ardhi na yanayo toka humo, na yanayo teremka kutoka
mbinguni, na yanayo panda humo. Naye yu pamoja nanyi popote mlipo. Na Mwenyezi
Mungu ni Mwenye kuyaona mnayo yatenda6.
Na hakika tumemuumba mtu,
nasi tunayajua yanayo mpitia katika nafsi yake7. Na Sisi tuko karibu naye kuliko mshipa wa
shingoni mwake.
Maelezo yanayopatikana
katika Aya hiyo.
Rejea:
[5] Surat Az-Zukhruf Aya ya 84
[6] Surat Al-Hadiyd Aya ya 4
[7] Surat Qaf Aya ya 16
Comments
Post a Comment