KHALIFA WA WAHABIA, HARUN RASHID
AMKASIRIKIA BAHLUL
Harun alimwajiri jasusi makhususi kwa
ajili ya kuchunguza na kuripoti kwake juu ya imani na akida sahihi za Bahlul.
Baada ya siku chache huyo jasusi alikamilisha uchunguzi wake na kuripoti kwa
Khalifa kuwa Bahlul alikuwa ni mpenzi wa Ahlal-Bayt wa Mtume (s.a.w.w.) na alikuwa
mfuasi wa Imam Musa al-Kadhim (a.s.) (imam wa saba wa Shia).
Harun alimwita Bahlul na kumwambia:
"Ewe Bahlul! Mimi nimepata habari za kuaminika kuwa wewe ni mmojawapo wa
wapenzi na wafuasi wakubwa wa Musa ibn Jaafar na hivyo unafanya kila jitihada
za kudhihirisha na hivyo umejidhihirisha u mwehu ambapo sivyo ulivyo!"
Bahlul alimjibu: "Iwapo hivyo ndivyo
ilivyo, je utanifanya nini?"
Kwa majibu hayo, Harun alighadhibika mno
na kumwamuru Masrur, mfanyakazi wake, amvue nguo Bahlul akalishwe juu ya punda
na kuzungushwa mjini na hatimaye kukatwa kichwa mbele yake Harun. Masrur,
alitekeleza vile alivyoamrishwa na hatimaye kumleta mbele ya Harun katika hali hiyo
ili aweze kuuawa.
Mara, hapo akatokezea Jaafer Barmaki
ambaye kwa kuiona hali hiyo ya Bahlul alimwuliza sababu ya hali yake hiyo:
"Ewe Bahlul! Je umetenda kosa
gani?" Bahlul alimjibu: "Kwa kuwa mimi nimesema ukweli, kwa hivyo
Khalifa akanizawadia mavazi yenye thamani."
Harun Rashid, Jaafar, na wote waliokuwepo
walichekeshwa mno kwa majibu ya Bahlul, na papo hapo Harun alimsamehe Bahlul na
kutoa amri ya kufunguliwa na apewe mavazi mapya na mazuri. Lakini Bahlul
hakukubali hayo bali yeye alichukua kifurushi cha nguo zake kuukuu na kuondoka.
MAZINGATIO
1. Watu wenye kudai kuwa ni waislamu
lakini kazi zao ni kuwaua waislamu sio mawahhabi pekee bali hata zamani walikuwepo.
Na Mtume na Ahlulbayt wake na wafuasi wao waliteswa sana na watu hawa ambao ni
wanafiki lakini wanalazimisha kuwaongoza waislamu kwa nguvu.
2. Ukiwa mwislamu wa kweli unapigwa
vita kutoka pande zote ndani ya Uislamu na nje ya Uislamu. Hivyo kunahitajika
uvumilivu wa hali ya juu kama aliokuwa nao Bahlul.
3. Uislamu sahihi ni upendo na
unapenda kuona wanadamu wote wanaishi kwa amani kinyume na juhudi zinazofanywa
na waislamu bandia. Hivyo tuwe waislamu sahihi na wapenda amani kwa watu wote
ili dunia iwe eneo salama kwa kuishi.
Comments
Post a Comment