KINA CHA DHATI CHA UTAKASO WA ALLAH (S.W) KIMEFICHIKANA KWA WATU WOTE.

KINA CHA DHATI CHA UTAKASO WA ALLAH (S.W) KIMEFICHIKANA KWA WATU WOTE.
Sisi tuna amini ya kuwa; japokuwa athari ya kuwepo Mwenyeezi Mungu imeenea katika ulimwengu wote, lakini uhakika wa dhati ya Mwenyeezi Mungu ni jambo lisilo wazi kwa mwanaadamu yeyote yule, na hakuna mtu yeyote yule anayeweza kufahamu kina cha dhati ya Mwenyeezi Mungu, kwa sababu dhati yake Mola Mtakatifu haina mwisho, na imeizunguka kila kitu na sisi wanaadamu tuna mipaka maalumu, mipaka ambayo ina mwisho wake, na ni kwa sababu hiyo basi, sisi hatuwezi kuifikia dhati yake.
Ama wao wamo katika shaka ya kukutana na Mola wao Mlezi! Ama hakika Yeye amekizunguka kila kitu.6
Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.7
Katika hadithi maarufu ya Mtume Muhammad (s.a.w.w) tunasoma, ya kuwa Nabii Muhammad (s.a.w.w) amesema:-
Kwa hakika sisi hatujakuabudu Wewe vile unavyostahiki kuabudiwa, na hatujakufahamu Wewe kwa uhaki, kama vile ilivyo haki yako kutambulika.8
Ama ni lazima tuzingatie kuwa; kauli hiyo haimaanishi kuwa kwa sababu hatuna elimu ya kuufahamu udhati wa ndani wa Mwenyeezi Mungu, basi vile vile hatuna elimu ya kumfahamu Mwenyeezi Mungu kijumla jamala, kwa hakika jambo hilo halikubaliki, kwa sababu Mwenyeezi Mungu ameviteremsha vitabu vyake ili kuwaletea wanaadamu elimu ya kumtambua Mola wao, na kwa kupitia vitabu hivyo wanaadamu huongoka na kufikia katika saada, tunaweza tukaashiria vitabu vingi kuhusiana na kauli hiyo, kwa mfano, sisi hatufahamu uhakika wa roho, ama kwa upande mwingine tuna elimu ya jumla jamala inayotuthibitishia kuwa roho ipo na tunaishuhudia.
REJEA:
[6] Surat Fussilat Aya ya 54
[7] Suratul-Buruuj Aya ya 20

[8] Buharul-Anwar, juzuu ya 68,uk23.

Comments