KUFUNGWA MILANGO YA NYUMBA ZA MASAHABA

KUFUNGWA MILANGO YA NYUMBA ZA MASAHABA
Nasai ametoa katika kitabu chake Khasais fi Fadhail Ali bin Abi Talib, hadith iliyopokelewa na Zaid bin Arqam kwamba milango ya baadhi ya nyumba za masahaba ilikuwa ikifungukia ndani ya msikiti (yaani wakitoka nyumbani mwao na kuingia msikitini moja kwa moja) Masjid Nabi.

Mtume (s.a.w.w) alitoa amri milango yote ifungwe isipokuwa mlango wa imam Ally (a.s). Masahaba wakaonyesha uchungu na kutoridhika kwa amri hii. Ndipo Mtume (s.a.w.w) akasimama na kuwahutubia. Baada ya kumsifu Mola akasema, “kwa Mujibu wa amri ya Mwenyezi Mungu nilikuamrisheni kuifunga milango yenu na Ali aiweke wazi; hoja na mabishano yenu hayatakiwi. Sikufunga wala kufungua mlango wa mtu yeyote kwa hiari yangu, bali nilifuata kama nilivyoamrishwa na Mwenyezi Mungu.
MFUNZO;
Hii hadith inatufundisha kuwa ubishi dhidi ya mafundisho na amri za Mtume hazikuanza leo, bali tokea enzi za masahaba, baadhi yao walikuwa wakimbishia Mtume bila kuona haya. Hivyo basi tujiepushe kuwafuata masahaba wabishi tusije kuangamia.
Pili tunajifunza kuwa Imam Ally (a.s) alikuwa na cheo maalumu kwa Allah na Mtume wake. Hakuna sahaba yeyote aliyefikia heshima na cheo alichopewa Imam Ally. Wote wanaojipandisha cheo juu ya imam Ally ni wapotoshaji na wamo katika kundi la wabishi waliokuwa wakimbishia mtume kila alipotoa amri hususani kuhusu uongozi wa Imam Ally (a.s).

Tatu: tufanye juhudi ili tuwe pamoja na Imam Ally (a.s) kwani hadith hii inaonyesha kuwa alikuwa amekwisha ridhiwa na Allah na hivyo tukimfuata yeye tutakuwa tumefuata njia sahihi. Na kumpinga ni sawa na kuingia katika lile kundi la wabishi.

Comments